Archive Pages Design$type=blogging

MCHUNGAJI ATOROSHA MKE WA MTU!

MCHUNGAJI anayejiita nabii na mtume, raia wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC) aliyetajwa kwa jina moja la Emmanuel amejikuta nd...

MCHUNGAJI anayejiita nabii na mtume, raia wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC) aliyetajwa kwa jina moja la Emmanuel amejikuta ndani ya majanga kufuatia madai mazito kwamba amemtorosha mke wa mtu ambaye ni mwimbaji wa Nyimbo za Injili Bongo anayekuja juu kwa kasi, Janet Mrema.

 
Mwimbaji wa Nyimbo za Injili Bongo anayekuja juu kwa kasi, Janet Mrema anayedaiwa kutoroshwa na mchungaji huyo.
Kwa mujibu wa chanzo makini, mchungaji huyo alifika nyumbani kwa Jonas Mrema, mume wa Janet, maeneo ya Tegeta-Nyaishozi jijini Dar na kuishi kama mtumishi wa Mungu lakini polepole alianza mazoea tata na Janet.
“Mume alianza kuhisi mabadiliko ya mkewe kwa mtumishi huyo, lakini nadhani aliona ni mawazo yake tu. Ndipo siku ya siku akashangaa mkewe na mchungaji huyo wameondoka nyumbani hapo.
“Kwa sasa tangu tukio hilo litokee ni miezi kama mitatu. Mume alihangaika sana kumtafuta mkewe hadi jana (Jumatatu iliyopita) ndipo akampata wakiwa na mchungaji huyo kwenye nyumba moja ambako walikuwa wakiishi pamoja,” kilisema chanzo chetu.
 
Katibu wa Chama cha Waimba Injili Tanzania, Stela Joel akilizungumzia sakata hilo.
Iliidaiwa kwamba, mchungaji huyo alipopekuliwa alikutwa na paspoti ya nchini Burundi wakati yeye ni Mkongo wa Uvira na alionekana kuishi nchini kinyume na sheria hivyo alifunguliwa jalada la kesi kwenye Kituo cha Polisi cha Wazo Hili, Tegeta lenye Kumbukumbu Na. WH/RB/7040/2014- KUISHI NCHINI BILA KIBALI.
Juzi, Amani liliwasiliana na Katibu wa Chama cha Waimba Injili Tanzania, Stela Joel ambaye alikiri kutokea kwa tukio hilo na kusema tayari chama hicho kimemsimamisha uanachana Janet kwa kitendo chake hicho cha kumtoroka mumewe wa ndoa.
“Ni kweli na Chama cha Waimba Injili Tanzania kimemsimamisha uanachama Janet. Hatuna mzaha katika maadili,” alisema Stela.Amani lilimpigia simu mume wa Janet, Jonas Mrema ambapo katika mazungumzo baada ya salamu alipewa pole kwa matatizo ya mkewe, alisema asante kisha alipoulizwa kuhusu hali ilivyo aliomba apige simu yeye baadaye kwa vile alikuwa kikaoni.
Hata hivyo, baada ya saa mbili kupita bila kupiga, Amani lilimpigia tena simu ambapo iliita bila kupokelewa hivyo jitihada za kumpata zinaendelea.
CHANZO:GPL

COMMENTS

Name

Burudani Habari Hot News Magazeti Majuu Michezo Teknolojia/Movie Track (Audio & Video)
false
ltr
item
Tabasam Blog: MCHUNGAJI ATOROSHA MKE WA MTU!
MCHUNGAJI ATOROSHA MKE WA MTU!
http://api.ning.com:80/files/HbsRLQ*GNXbEAtRXUYQvGr5xvdwg0-sMK6APrdzZpwef3hRjXjmEogavP2jGtI8EB1CaZvPcZl*pWv4YdtME3yPS4XT3nUqb/DSC_0134.JPG?width=650
Tabasam Blog
https://tabasmtza.blogspot.com/2014/10/mchungaji-atorosha-mke-wa-mtu.html
https://tabasmtza.blogspot.com/
http://tabasmtza.blogspot.com/
http://tabasmtza.blogspot.com/2014/10/mchungaji-atorosha-mke-wa-mtu.html
true
939923276739022787
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago