Tanzania ina wanachama hai zaidi ya 600 wa kundi la watu wenye imani ya siri ya Freemas...
Tanzania
 ina wanachama hai zaidi          ya 600 wa kundi la watu wenye imani ya
 siri ya Freemasons wakiwa          wanatokana na watu wa kada 
mbalimbali wakiwemo maarufu, huku          ikielezwa kwamba miongoni 
mwao hakuna viongozi wakuu wa          serikali.
Hayo
 yalibainishwa na Kiongozi wa          kundi la Freemasons katika eneo 
la Afrika Mashariki, Jayantilal          Keshavji Chande maarufu kama 
Sir Andy Chande.
Kiongozi 
huyo Mtanzania mkazi wa          Dar es Salaam mwenye asili ya Kiasia, 
alisema licha ya Tanzania          kuwa na wanachama hao, kwa sasa idadi
 ya wanachama duniani          inapungua tofauti na inavyoonekana sasa 
kuwa wanaongezeka          kutokana na kuibuka maneno mengi kuhusu kundi
 hilo.
Alisisitiza kuwa si
 rahisi kumjua          mwanachama wa kundi hilo, bali wenyewe ndio 
wanaofahamiana,          akisema ni siri na kwamba wenyewe wanakutana 
katika vikao          mbalimbali mara moja kwa mwezi au zaidi.
Alisema
 nchini kuna wanachama          zaidi ya 600 wakiwemo wafanyabiashara, 
watumishi serikalini,          walimu pamoja na wanataaluma mbalimbali 
wanaoheshimika sana na          kusisitiza kuwa kuna maneno mengi 
yanayosemwa kuhusu kundi hilo,          ambayo siyo ya kweli.
Alisema
 idadi ya wanachama wake          duniani inazidi kupungua kutoka 
milioni nane hadi sasa wako          milioni sita, tofauti na wengi 
wanaodhani kuwa idadi hiyo          inaongezeka.
Chande
 alizungumza na mwandishi          wa habari hizi katika Shule ya 
Sekondari ya Shaaban Robert          ambako yeye ni Mwenyekiti wa Bodi 
ya shule alipozungumzia          maadhimisho ya miaka 50 tangu 
kuanzishwa kwake.
Alisema 
duniani kuna watu wazito          wengi ambao ni wanachama wa kundi hilo
 kama majaji wakubwa na          hata Binamu wa Malkia Elizabeth wa 
Uingereza ni kiongozi mkubwa          wa kundi hilo.
Akizungumzia
 masharti ya kujiunga          na kundi hilo, Chande alisema ni lazima 
mwanachama huyo awe          anaamini katika Mungu bila kubagua iwapo ni
 Mkristo au Muislamu.
Alisema
 pia ni lazima anayetaka          kujiunga awe na umri unaozidi miaka 21
 na walio chini ya umri          huo hawaruhusiwi kujiunga na lazima 
familia ya anayetaka          kujiunga na wanandugu wafahamu kuwa 
umejiunga na kundi hilo.
"Unajua
 katika imani hii kuna          michango mbalimbali ambayo unatakiwa 
kutoa ambayo ni zaidi ya          dola milioni sita (karibu Sh bilioni 
10), hivyo ni lazima ndugu          wafahamu ili kuepuka matatizo 
utakapotakiwa kutoa," alisisitiza.

Alisema
 si kweli kuwa wenye fedha          wengi ni wanachama wa kundi hilo 
huku akikanusha wanachama          wanajiunga kwa ajili ya kupata fedha,
 bali ni dini kama imani          nyingine.
Alisisitiza
 kuwa hakuna ukweli          kwamba wanaopata mafanikio katika maisha 
wakiwa ndani ya imani          ya Freemasons kuwa wanatoa kafara watu 
wao wa karibu kwa lengo          la kupata utajiri.
Chande
 pia alisema hairuhusiwi          kutumia jina la kundi hilo kwa nia ya 
kujipatia nafasi sehemu          mbalimbali au kuongeza nafasi katika 
chuo au shule.