Mapenzi ya Rihanna kwenye soka yameingia katika hatua nyingine na sasa hataki kuwa shabiki tu bali mmiliki halali wa t...
Mapenzi ya Rihanna kwenye soka yameingia katika hatua nyingine na sasa hataki kuwa shabiki tu bali mmiliki halali wa timu kubwa duniani, na kwa kuanza anataka kuinunua Liverpool FC!
Kwa mujibu wa gazeti la Hispania, El Mundo Deportivo mwimbaji huyo
alianza mpango huo muda mfupi baada ya kuisha kwa fainali za kombe la
dunia nchini Brazil ambapo alionekana akitweet mara kwa mara kuhusu
mechi zilizokuwa zinaendeelea.
Gazeti hilo limeeleza kuwa Rihanna amekuwa akipata ushauri kutoka kwa
marafiki zake wa karibu akiwemo mchezaji wa Chelsea, Didier Drogba ili
kufanya maamuzi sahihi katika ununuzi wa club ya mpira wa miguu.

Kwa sasa Liverpool inamilikiwa na John W. Henry na hana mpango wa kuiuza timu hiyo ya soka.