post-feature-image
HomeBurudani

‘MTOTO WA NDEGE’ AOKOKA

MTOTO Happiness Lyoba (10) ambaye aliripotiwa kuwa mwingi wa vituko vya maajabu, ...

LULU AMLEGEZEA MKONGO
MENEJA WA T.I ATINGA LEADERS KUSHUHUDIA MAANDALIZI YA SHOO YA SERENGETI FIESTA 2014
Hiki Ndicho alichokisema Fid Q baada ya watu kuendelea kuuzungumzia umri wa Miss Tanzania Sitti Mtemvu?

MTOTO Happiness Lyoba (10) ambaye aliripotiwa kuwa mwingi wa vituko vya maajabu, ikiwamo kuonekana akishuka katika ndege huko Zanzibar, ameripotiwa kuokoka katika Kijiji cha Mkokozi, wilayani Mkuranga, Pwani.
Mtoto Happiness Lyoba (10) akisoma Biblia.
Akizungumza na gazeti hili, mama wa mtoto huyo, Salah Zefania alisema mwanaye huyo alitoroka tena Septemba 16, mwaka huu na kukamatiwa eneo la Feri jijini Dar es Salaam, akidai kuwa ameitwa  na baba yake.
Baada ya kumkamata na kuanza kurejea naye kijijini Mkokozi ambako amehifadhiwa na msamaria mwema, alisema alipata simu nyingi za watu kumpa pole kwa tukio hilo, hali iliyomshangaza kwani hakuelewa watu hao walipataje habari hizo.
Mama mzazi wa mtoto Happiness Lyoba , Salah Zefania.
Miongoni mwa simu hizo ni pamoja na ya Mwinjilisti wa kanisa lao la Kisabato Mbagala aliyemtaja kwa jina la Jacob Mayala ambaye alihitaji kumuombea mtoto wake. ‘’Ni kweli Mwinjilisti huyo alifika Mkokozi na kufanya maombi maalumu yaliyoambatana na kufunga kwa siku kadhaa. Hali ya mwanangu kwa sasa ninakubaliana nayo maana amegeuka kuwa  binadamu ambaye  nilimtarajia, Happiness  hakuwa hivi maana alizidisha vituko vya maajabu,” alisema.
Mtoto Happiness Lyoba akiwa na mama yake.
Mama huyo amewaomba Watanzania wamsaidie mwanaye kusoma kwani hivi sasa anajitambua tofauti na huko nyuma.“Mimi kipato changu ni kidogo na huku niliko ni mbali sana, hakuna shule karibu, kazi yangu ni kilimo cha mbogamboga na tena hapa ninapoishi nimehifadhiwa tu, ninaomba msaada ili mtoto wangu aende shule,” alisema mama huyo akidai kuwa Ustawi wa Jamii ulimshauri kumweka binti yake mbali na maeneo aliyokuwa akiishi.
“Nilishauriwa asirudi  Kitunda kwa muda huu maana huko ndiko alikoanza kupatwa na hali ambayo naamini ilikuwa ni mapepo,” alisema.
Mtoto na mama wakisali pamoja.
HAPPINES  LYOBA
Kwa upande wake, Happines alisema anahitaji kusoma na kwamba matukio aliyokuwa akiyafanya hakujua yalivyotokea.
Mtu yeyote aliyeguswa na hali ya mtoto huyu ambaye akili yake imerejea kuwa ya kawaida kufuatia maombi ya kila siku, anaweza kuwasiliana na mama yake kwa namba 0768 632693.
Name

Burudani Habari Hot News Magazeti Majuu Michezo Teknolojia/Movie Track (Audio & Video)
false
ltr
item
Tabasam Blog: ‘MTOTO WA NDEGE’ AOKOKA
‘MTOTO WA NDEGE’ AOKOKA
http://api.ning.com:80/files/06WphArD*MsXIiqNihhcuzd31C5yCQ-ElBMsamx3tPo8Lun28CcY01uDfpBe1CrF1yzc1zhtfPHsKcmsTGSl0hAUMJHCLBjO/IMG_1131.jpg
Tabasam Blog
https://tabasmtza.blogspot.com/2014/11/mtoto-wa-ndege-aokoka.html
https://tabasmtza.blogspot.com/
http://tabasmtza.blogspot.com/
http://tabasmtza.blogspot.com/2014/11/mtoto-wa-ndege-aokoka.html
true
939923276739022787
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago