post-feature-image
HomeBurudani

DIAMOND, ZARI GUMZO AIRPORT

  Musa Mateja na Imelda Mtema BAADA ya kula bata za kutosha Bongo, wakati wakisindikizana kimahaba, staa wa Bongo Fle...

Huyu Ndio Msanii wa Nigeria aliyefanya collabo na Rihanna
MSINISHANGAE KUFUNGA RAMADHANI - PENNY
UWOYA ATOKA NDUKI HOTELINI
 
Musa Mateja na Imelda Mtema
BAADA ya kula bata za kutosha Bongo, wakati wakisindikizana kimahaba, staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ na mrembo mkali kutoka Uganda, Zarinah Hassan a.k.a Zari au The Boss Lady, wamezua gumzo kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar, Ijumaa lina mchapo kamili.

Mrembo mkali kutoka Uganda, Zarinah Hassan a.k.a Zari au The Boss Lady (mwenye gauni jekundu) akishuka kutoka gari la ‘Diamond Platnumz’.
HABARI KAMILI
Tukio hilo lililoshuhudiwa na wanahabari wetu lilijiri mishale ya mchana, Jumanne iliyopita katika maegesho ya airport (uwanja wa ndege) ambapo Diamond alikuwa akimsindikiza Zari aliyekuwa akitimua Bongo baada ya kufanya yao kwa siku kadhaa.
KABLA YA TUKIO
Awali kabla ya tukio hilo, gazeti hili lilipokea ‘ubuyu’ kutoka kwa chanzo chake cha kuaminika kwamba, wawili hao walikuwa wakijiandaa katika hoteli waliyokuwa kwa siku kadhaa iliyopo kwenye Ufukwe wa Bahari ya Hindi, tayari kuelekea uwanja wa ndege.

Zari au The Boss Lady akimwelekeza kitu mpambe wa 'Diomond'.
“Ijumaa acheni kulaza damu, kwa taarifa yenu Diamond ndiyo anajiandaa kumpeleka Zari airport wahini pale mpate tukio kamili ili kumaliza ubishi kuwa kweli walikuwa wote Bongo,” kilisema chanzo hicho kikiomba hifadhi ya jina gazetini.
IJUMAA MZIGONI
Baada ya kunyetishiwa ishu hiyo, wanahabari wetu walitia gia kwenye ‘motokaa’ ambapo dakika kadhaa baadaye walikuwa wametega satelaiti zao uwanjani hapo tayari kwa kunasa tukio.

Gari jeusi aina ya BMW X6 ya mkali 'Diamond' ikiendeshwa na mpambe wake aliyejulikana kwa jina la Q-Boy huku mwenyewe (Diamond) siti ya nyuma.
BMW X6 LATOKEA
Wakati wanahabari wetu wakiwa wanakaribia kukata tamaa, ghafla lilitokea gari jeusi aina ya BMW X6 ambalo tofauti na magari mengine, badala ya namba za usajili, lenyewe lilikuwa na maandishi yaliyosomeka kwa herufi kubwa ‘PLATNUMZ’ kisha likapaki kwenye eneo la maegesho uwanjani hapo.
Gari hilo lilikuwa likiendeshwa na kijana mmoja wa Diamond aliyejulikana kwa jina la Q-Boy na pembeni mwake kwenye siti ya abiria alikuwepo mpambe mwingine wa msanii huyo ambaye jina halikupatikana.
DIAMOND AJIFUNGIA
Wakiwa siti ya nyuma, wakati Zari anashuka, Diamond alijifungia kwenye gari ili kuwakwepa mapaparazi baada ya kuwashtukia kuwa walikuwa wakimsubiri.

Zari au The Boss Lady akisindikizwa na mpambe wa 'Diamond'.
WAZUA GUMZO
Wawili hao walizua gumzo uwanjani hapo ambapo baadhi ya watu wakiwemo Wazungu walikuwa wakiwashangaa huku Wabongo wakitamani Diamond atoke kwenye gari amtambulishe Zari kama ndiye mrithi wa Wema au la!
“Huyu Diamond naye balaa. Kampata wapi mtoto mrembo kiasi hiki? Hakyanani na mimi bora niwe msanii nitafaidi. Mtoto kaumbika hasa,” alisikika mmoja wa madereva teksi huku wenzake wakimkatisha tamaa kuwa hawezi kuwa msanii. Zari alishuka na yule mpambe wa Diamond na kuambatana hadi sehemu ya kukaguliwa ili akapande ndege.

Zari, 'The Boss Lady' akilonga jambo na paparazi wa gazeti la Ijumaa.
IJUMAA LAMBANA ZARI
Kabla ya kufikia sehemu hiyo, wanahabari wetu walibahatika kumfotoa picha za kutosha Zari kisha kumfuata na kumuuliza alikuwa na ishu gani na Diamond ambaye alikuwa naye hotelini Bongo kwa takriban siku tano.
Hata hivyo, Zari alishindwa kujibu na kuishia kusema kuwa hana maoni.“No comment,” alisema Zari na hata alipoombwa kufafanuzi kidogo aligoma.
DIAMOND AFUNGUKA
Baada ya tukio hilo, wanahabari wetu walimtafuta Diamond kwa njia ya simu ili azungumzie kwa kina juu ya uwepo wa Zari Bongo na tuhuma za kujihusisha naye kwenye mapenzi ambapo Diamond alifunguka:

Mbongo Fleva 'Diamond' wakati akitanua na Zari, 'The Boss Lady'.
“Niliwaona airport mkimpiga picha na gari langu na mkaongea naye.
“Kweli ninyi ni noma sana, lakini nadhani mliandika hivi karibuni kuwa mimi nimeachwa na Wema (Sepetu).
“Ukweli hakuna mwanaume anayeweza kujitoa kwa demu wake hasa kumpatia zawadi ya gari kama niliyotoa kwenye bethidei ya Wema halafu baadaye usikie kuna mwanaume mwingine katoa zaidi na ukaendelea kufurahia.
ZARI NI RAFIKI TU JAMANI!
“Sitaki kuongea mengi ila Zari naomba atambulike kama rafiki yangu tu jamani.”
YATOKANAYO
Hivi karibuni Diamond alimwagana na Wema ambapo siku chache baadaye habari zilivuja kwamba Zari ambaye ni msanii wa kike tajiri Afrika Mashariki ndiye mwenye uwezo wa kuziba pengo hilo mara tu baada kuonekana na jamaa huyo.
CHANZO: IJUMAA /GPL
Name

Burudani Habari Hot News Magazeti Majuu Michezo Teknolojia/Movie Track (Audio & Video)
false
ltr
item
Tabasam Blog: DIAMOND, ZARI GUMZO AIRPORT
DIAMOND, ZARI GUMZO AIRPORT
http://api.ning.com:80/files/j-DiiE-nbb80*rVSrQ7MKMDtnEVhIaZuSe9oeGWd4Je1J56MLUecJyWB-45XQu-3HZbf*ouVZ5eVKNiHYuT9kOa9H3I40FQ2/IMG_0047.JPG
Tabasam Blog
https://tabasmtza.blogspot.com/2014/11/diamond-zari-gumzo-airport.html
https://tabasmtza.blogspot.com/
http://tabasmtza.blogspot.com/
http://tabasmtza.blogspot.com/2014/11/diamond-zari-gumzo-airport.html
true
939923276739022787
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago