Archive Pages Design$type=blogging

ESHE BUHETI: NAMVALIA KHANGA MOKO MUME WANGU TU

Katika safu hii wiki hii tunaye mwanadada anayeyaendesha maisha yake kwa kuuza su...

Katika safu hii wiki hii tunaye mwanadada anayeyaendesha maisha yake kwa kuuza sura kwenye filamu Bongo. Huyu si mwingine bali ni Eshe Buheti.
Mkali katika tasnia ya filamu Bongo, Eshe Buheti.
Kama ilivyo ada naye aliwekwa mtukati na mwandishi wetu Imelda Mtema na kuulizwa maswali ambayo alitoa ushirikiano katika kuyajibu.Ijumaa: Unaonekana kutoandamwa na skendo kama inavyokuwa kwa mastaa wengine, hii inatokana na nini?
Eshe: Unajua mimi ni mke wa mtu, najichunga sana kuhakikisha sichafuki kwa namna yoyote, ndiyo maana unaona skendo zinanipitia mbali.
Ijumaa: Hebu tuambie, unapokuwa nyumbani unapendelea kuvaa mavazi gani?
 Eshe: Nikiwa ndani kwangu hasa na mume wangu akiwepo ni mwendo wa khanga moja kwa kwenda mbele.
Ijumaa: Mastaa mbalimbali inakuwa vigumu kuolewa na wakiolewa hawadumu kwenye ndoa zao, wewe unadhani utadumu?
Eshe: Kila jambo anapanga Mungu, kikubwa najitahidi kumheshimu mume wangu na kumfanyia kila linalomfurahisha na kuacha yanayomkera, naamini kwa kufanya hivyo ndoa yetu itadumu.
Ijumaa:  Najua una mtoto mmoja sasa, vipi una mpango wa kuongeza mwingine soon?
Eshe: Mwanangu anaonesha kabisa anataka mdogo wake, kwa hiyo tunajipanga na naamimi hatuna muda mrefu tutafanya maandalizi ya kumleta kiumbe mwingine duniani.
Ijumaa: Wanaume wengi hawapendi kazi ya usanii hasa kutokana na skendo mbalimbali, vipi wewe mume wako amewezaje kukubaliana na kazi yako?
Eshe: Nahisi mume wangu ni mtu wa tofauti, ananiamini na kwa kuwa hajawahi kusikia lolote baya, wala hana wasiwasi.
Ijumaa: Kuna mastaa ambao wana katabia ka’ kuiba waume za watu, siku ukijua kuna anayemnyemelea mumeo utafanyaje?
 Eshe: Huyo atakuwa ananitafuta shari na kwa kweli ajiandae kwa mpambano. Siwezi kuingiliwa kwenye anga zangu halafu nione sawa tu.
Ijumaa:  Kutokana na tabia ya mastaa wengi kuwa na kucha ndefu na kutopenda kiziharibu hata kupika hawawezi, wewe kwako hili likoje?
Eshe: Kwa mambo ya mahanjumati yani hapa ndiyo umefika, omba siku nikualike uje kula kwangu ndiyo utajua mimi ni mpishi au mbabaishaji.
Ijumaa: Ni mambo gani ambayo huyapendi kabisa kwenye maisha yako?
Eshe:  Mimi sipendi umbeya, uvivu, majungu kwani ni vitu ambavyo vinaturudisha nyuma.
Ijumaa: Kwenye sanaa kuna vishawishi vingi sana hasa hii tabia ya baadhi ya maprodyuza kupenda sana rushwa ya ngono, wewe unakabiliana vipi na changamoto hiyo?
 Eshe: Najitambua na ninajiheshimu sana. Siwezi kujivunjia heshima yangu kwa mambo ya kijinga kwa hiyo Mungu ananisaidia navuka changamoto hizo.
Ijumaa: Unawashauri vipi hawa mastaa ambao mabifu ni sehemu ya maisha yao?
Eshe: Hili ni tatizo na kwa kweli ni vyema sisi mastaa tukawa na umoja na tukashirikiana katika kuendeleza sanaa yetu badala ya kugombana.

COMMENTS

Name

Burudani Habari Hot News Magazeti Majuu Michezo Teknolojia/Movie Track (Audio & Video)
false
ltr
item
Tabasam Blog: ESHE BUHETI: NAMVALIA KHANGA MOKO MUME WANGU TU
ESHE BUHETI: NAMVALIA KHANGA MOKO MUME WANGU TU
http://api.ning.com:80/files/UxG8FbEp4zbAfeTOo2*cfNkqn0uP5CchpjIOcIBr-IRrEEWYEHg5aRl0qBRTX0fP24wt68yFzfJ6Qhyte-E1pyyNQWSpVong/buhe.jpg
Tabasam Blog
https://tabasmtza.blogspot.com/2014/12/eshe-buheti-namvalia-khanga-moko-mume.html
https://tabasmtza.blogspot.com/
http://tabasmtza.blogspot.com/
http://tabasmtza.blogspot.com/2014/12/eshe-buheti-namvalia-khanga-moko-mume.html
true
939923276739022787
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago