Stori: Waandishi Wetu NYOTA yake inang’ara hata mchana, siku hadi siku anazidi kuwa...
Stori: Waandishi Wetu NYOTA
yake inang’ara hata mchana, siku hadi siku anazidi kuwa wa kimataifa
zaidi. Awali walisema anang’aa kwa sababu ana uhusiano wa kimapenzi na
Miss Tanzania, 2006, Wema Sepetu lakini juzikati wamemwagana, jamaa bado
yuko juu! Watu wanauliza, ni mchawi?
Kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) jijini Dar, Diamond alilakiwa na maelfu ya mashabiki wake ambao wengi walikuwa wakihoji kung’aa kwake kunatokana na nini!
“Jamani watu ni wengi sana, mimi nataka kuwaambia huyu Diamond si ajabu anatumia uchawi.
Mimi natokea Sinza Mori jirani na kwa mama yake Diamond, sijala hadi muda huu (saa 8:25) lakini sina njaa nataka tu kumwona Diamond,” alisikika akisema mmoja wa mashabiki waliofurika uwanjani hapo.
Mwingine alisema inawezekana Diamond akawa anatumia ‘kizizi’ kwani hakuna Mbongo Fleva aliyeng’aa kwa muda mrefu kama yeye na kila siku anazidi kwenda juu badala ya kushuka.
...Mamia ya mashabiki wakimshangilia staa huyo.
ALIVYOTUA
Baada ya Diamond kuwasili, msafara wa kutoka uwanjani kuelekea mjini ulianza ambapo alipitia Buguruni- Chama. Alipofika hapo Diamond alishuka kwenye gari na kutembea kwa miguu kitendo kilichowafurahisha mashabiki wake kumwona msela ‘anapiga maguu’.
“Huyu ndiyo shujaa wetu wa kweli, hata kama wengine wanasema kuwa si nguvu za kawaida zinazomuweka juu lakini jamaa anajua kujituma,” alisikika mmoja wa mashabiki waliofurika Buguruni.
WAELEKEA MAGOMENI
Baada ya kumalizana na watu wa Buguruni, Diamond akiwa amezungukwa na umati, aliendelea kutembea kwa miguu hadi Ilala-Mchikichini, akapanda bodaboda kuelekea Kariakoo huku gari lake likimfuata kwa nyuma.
Umati wa watu ukimsindikiza mkali huyo.
Mapaparazi wetu waliendelea kuufatilia msafara huo ambao ulitikisa
jiji kutokana na idadi kubwa ya watu kuguswa na kuufuata kiasi ambacho
ilibidi polisi waingilie kati.“Afadhali polisi wameingilia kati maana
pengine watu wangeweza kuuana le hapa,” alisema Juma Dodi, mkazi wa
Kariakoo.
POLISI WAMVUSHA
Kuonesha kwamba wanajali, Polisi wa Kituo cha Msimbazi jijini Dar, walilazimika kumvusha nyota huyo kutoka Kariakoo kwa kutumia ‘difenda’ lao hadi maeneo ya Jangwani wakamuacha aendelee na msafara wake kwa kutumia gari lake aina ya Toyota Prado.
WAELEKEA TANDALE
Msafara huo ulioambatana na bodaboda, magari mengi ya wadau wa muziki Bongo, ulielekea moja kwa moja nyumbani kwao Tandale na kukaa kwa muda mfupi huku kila mtu ‘Diamond Diamond huku watu waliotarajiwa kupiga buu (Timu Wema) wakiingia mitini.
Nyota wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’.
Baada ya hapo, msafara ukaanza tena kuaelekea ukumbi maarufu wa
burudani ya Escape One uliopo Mikocheni jijini Dar kwa ajili ya mkutano
maalum na waandishi wa habari.
Diamond alishinda tuzo hizo akiwa ameshindana na wasanii kibao kutoka sehemu mbalimbali barani Afrika.
Nyota wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ akifurahia tuzo alizojinyakulia huko Sauzi.
Huyu si mwingine ni nyota wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’
ambaye juzi alitua nchini akitokea Afrika Kusini ‘Sauz’ alikoshinda tuzo
3 za Channel O zilizofanyika jijini Johannesburg nchini humo mwishoni
mwa wiki iliyopita.Kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) jijini Dar, Diamond alilakiwa na maelfu ya mashabiki wake ambao wengi walikuwa wakihoji kung’aa kwake kunatokana na nini!
“Jamani watu ni wengi sana, mimi nataka kuwaambia huyu Diamond si ajabu anatumia uchawi.
Mimi natokea Sinza Mori jirani na kwa mama yake Diamond, sijala hadi muda huu (saa 8:25) lakini sina njaa nataka tu kumwona Diamond,” alisikika akisema mmoja wa mashabiki waliofurika uwanjani hapo.
Mwingine alisema inawezekana Diamond akawa anatumia ‘kizizi’ kwani hakuna Mbongo Fleva aliyeng’aa kwa muda mrefu kama yeye na kila siku anazidi kwenda juu badala ya kushuka.
Baada ya Diamond kuwasili, msafara wa kutoka uwanjani kuelekea mjini ulianza ambapo alipitia Buguruni- Chama. Alipofika hapo Diamond alishuka kwenye gari na kutembea kwa miguu kitendo kilichowafurahisha mashabiki wake kumwona msela ‘anapiga maguu’.
“Huyu ndiyo shujaa wetu wa kweli, hata kama wengine wanasema kuwa si nguvu za kawaida zinazomuweka juu lakini jamaa anajua kujituma,” alisikika mmoja wa mashabiki waliofurika Buguruni.
WAELEKEA MAGOMENI
Baada ya kumalizana na watu wa Buguruni, Diamond akiwa amezungukwa na umati, aliendelea kutembea kwa miguu hadi Ilala-Mchikichini, akapanda bodaboda kuelekea Kariakoo huku gari lake likimfuata kwa nyuma.
POLISI WAMVUSHA
Kuonesha kwamba wanajali, Polisi wa Kituo cha Msimbazi jijini Dar, walilazimika kumvusha nyota huyo kutoka Kariakoo kwa kutumia ‘difenda’ lao hadi maeneo ya Jangwani wakamuacha aendelee na msafara wake kwa kutumia gari lake aina ya Toyota Prado.
WAELEKEA TANDALE
Msafara huo ulioambatana na bodaboda, magari mengi ya wadau wa muziki Bongo, ulielekea moja kwa moja nyumbani kwao Tandale na kukaa kwa muda mfupi huku kila mtu ‘Diamond Diamond huku watu waliotarajiwa kupiga buu (Timu Wema) wakiingia mitini.
Diamond alishinda tuzo hizo akiwa ameshindana na wasanii kibao kutoka sehemu mbalimbali barani Afrika.