Stori: Chande Abdallah na Deogratius Mongela Baada ya ile aibu ya kihistoria ya kuvu...
Stori: Chande Abdallah na Deogratius Mongela
Baada ya ile aibu ya kihistoria ya kuvua taji, inadaiwa kwamba yule Miss Tanzania 2014 aliyechakachua umri kisha kubwaga manyanga, Sitti Abbas Mtemvu, amerudi Marekani ili kukwepa masimango.
Miss Tanzania 2014 aliyechakachua umri kisha kubwaga manyanga, Sitti Abbas Mtemvu.
Kwa mujibu wa chanzo makini kilichoomba hifadhi ya jina, mrembo huyo
anadaiwa kukwea pipa (ndege) akiongozana na mama yake kisha kutua Texas,
Marekani ili kupoza machungu na kuepuka kero alizokuwa akikumbana nazo.
“Yaani walidhani tatizo wamelimaliza baada ya Sitti kujivua taji, kumbe ndiyo kwanza mengine yaliendelea kuibuka, wapo wanaotaka arudishe zawadi.
“Wengine wanataka afungwe kwa kudanganya umri jambo ambalo ni kosa kisheria na wengine walienda mbali zaidi wakidai ajivue pia Taji la Miss Temeke na lile la Chang’ombe.“Hayo yote yalimchanganya sana Sitti na familia yake ndiyo maana ameamua arudi zake Marekani kujipumzisha,” kilisema chanzo hicho.
Kikizidi kutiririka, chanzo hicho kilidai kuwa miss huyo alisafiri Novemba 16, mwaka huu, majira ya saa 9:00 alasiri kwa kificho ambapo alielekea nchini Marekani ambako ameishi kwa muda mrefu.
Baada ya kunyetishiwa ishu hiyo, wanahabari wetu waliwatafuta watu wa karibu wa Sitti ambapo walikataa kulizungumzia suala hilo kwa undani wakidai kuwa atafutwe Sitti mwenyewe ili azungumze.
Baada ya ile aibu ya kihistoria ya kuvua taji, inadaiwa kwamba yule Miss Tanzania 2014 aliyechakachua umri kisha kubwaga manyanga, Sitti Abbas Mtemvu, amerudi Marekani ili kukwepa masimango.
“Yaani walidhani tatizo wamelimaliza baada ya Sitti kujivua taji, kumbe ndiyo kwanza mengine yaliendelea kuibuka, wapo wanaotaka arudishe zawadi.
“Wengine wanataka afungwe kwa kudanganya umri jambo ambalo ni kosa kisheria na wengine walienda mbali zaidi wakidai ajivue pia Taji la Miss Temeke na lile la Chang’ombe.“Hayo yote yalimchanganya sana Sitti na familia yake ndiyo maana ameamua arudi zake Marekani kujipumzisha,” kilisema chanzo hicho.
Kikizidi kutiririka, chanzo hicho kilidai kuwa miss huyo alisafiri Novemba 16, mwaka huu, majira ya saa 9:00 alasiri kwa kificho ambapo alielekea nchini Marekani ambako ameishi kwa muda mrefu.
Baada ya kunyetishiwa ishu hiyo, wanahabari wetu waliwatafuta watu wa karibu wa Sitti ambapo walikataa kulizungumzia suala hilo kwa undani wakidai kuwa atafutwe Sitti mwenyewe ili azungumze.