post-feature-image
HomeBurudani

DAVINA NIWAPO CHUMBANI NI MWENDO WA NGUO LAINIII!

Leo kwenye safu yetu hii tunaye mwanadada kutoka kwenye tasnia ya filamu Bongo anayefahamika kwa jina la Davina lakini jina alilopew...

Nay wa Mitego Azungumza Haya Kuhusu Kuzaa na Siwema Baada ya Kupitia Mengi
Nalia Nikimaliza Kufanya Mapenzi..Naombeni Ushauri Jamani
KAJALA AJIUNGA RASMI FACEBOOK, AKAUNTI YAKE HII HAPA

Leo kwenye safu yetu hii tunaye mwanadada kutoka kwenye tasnia ya filamu Bongo anayefahamika kwa jina la Davina lakini jina alilopewa na wazazi wake ni Halima Yahaya.
Kama ilivyo ada naye anajibu maswali 10 yahusuyo maisha yake binafsi na kisanii ambayo paparazi wetu Hamida Hassan alimbana na aliyajibu kama ifuatavyo;
 
Mkali katika tasnia ya filamu bongo, Halima Yahaya 'Davina'.
Ijumaa: Najua una dada wa kazi, unapokuwa nyumbani huwa unafanya nini?
Davina: Licha ya kuwa na dada wa kazi, nikiwa nyumbani si mtu wa kukaa tu, napenda kufanya usafi wa nyumba yangu, kupika na kucheza na mtoto.
Ijumaa: Je, ni chakula gani unachopendelea kumpikia mumeo?
 Davina: Kiukweli mume wangu anapenda sana makaroni na nyama ya kusaga, ili kumfanya awe na furaha huwa nampikia chakula hicho.
Ijumaa: Ni sehemu gani ya mwili wako unayoipenda zaidi?
Davina: Sibagui, kila sehemu ya mwili wangu naipenda na namshukuru Mungu kwa kuniumba hivi nilivyo.
Ijumaa: Uwapo chumbani na mumeo, nguo gani ambazo unapendelea kumvalia?
 Davina: Hahaha, niwapo eneo hilo navaa nguo lainiii na vipensi ndiyo usiseme!
Ijumaa: Kiufupi wewe ni mrembo, unamvutia kila mwanaume, unajilinda vipi na vishawishi vya wanaume wakware?
Davina: Namshukuru Mungu kwa kunipa ndoa kwani ndiyo inanifanya naweza kuepuka vishawishi. Najiheshimu na kuiheshimu ndoa yangu.
Ijumaa: Ikitokea umebaini mumeo kakusaliti utachukua uamuzi gani?
Davina: Kwanza ni kitu ambacho sikitarajii kabisa kutokana na mapenzi anayonionesha na uaminifu alionao.
 
Davina akipozi.
Ijumaa: Kwa nini hivi sasa umekuwa ukiigiza sana sehemu ya mama tofauti na ilivyokuwa huko nyuma?
 Davina: Unajua hivi sasa mimi ni mama, kwahiyo ninapoigiza nafasi hiyo huwa navaa uhusika ipasavyo. Hata hivyo, nafasi nyingine pia huwa nafanya vizuri.
Ijumaa: Umejaaliwa kupata mtoto mmoja, je una mpango wa kuongeza mwingine na je unatarajia kuwa na familia ya watoto wangapi?
Davina: Siwezi kusema nahitaji familia ya watoto wangapi ila Mungu atakaonijaalia. Kwa sasa sina mpango wa kuongeza mwingine mpaka baadaye sana.
Ijumaa: Wewe umeolewa, unawazungumziaje wasanii wenzako ambao wana watu wao lakini wanachepuka tena wakati mwingine bila kificho?
Davina: Nihimize wasanii kujiheshimu na kuziheshimu ndoa zao, kama wana wapenzi basi watulie. Hii kurukaruka hasa katika ulimwengu wa sasa ni kujitafutia matatizo katika siku zijazo.
Ijumaa: Unayazungumziaje haya mabifu ndani ya Bongo Muvi?
Davina: Unajua maendeleo hayawezi kupatikana kwenye sanaa kama hatutakuwa kitu kimoja. Mabifu si kitu kizuri, mimi nasema tuna kila sababu ya kuondoa tofauti zetu.
Name

Burudani Habari Hot News Magazeti Majuu Michezo Teknolojia/Movie Track (Audio & Video)
false
ltr
item
Tabasam Blog: DAVINA NIWAPO CHUMBANI NI MWENDO WA NGUO LAINIII!
DAVINA NIWAPO CHUMBANI NI MWENDO WA NGUO LAINIII!
http://api.ning.com:80/files/j-DiiE-nbb88SN*dGYXrPO-wgGDk94UA7GQl4kdpmUrIckAIqOJXugplYTXscCWmlwXBw7vX0bRDiq40RlYWBlkwwGNMqnBg/DAVINA2.jpg?width=650
Tabasam Blog
https://tabasmtza.blogspot.com/2014/11/davina-niwapo-chumbani-ni-mwendo-wa.html
https://tabasmtza.blogspot.com/
http://tabasmtza.blogspot.com/
http://tabasmtza.blogspot.com/2014/11/davina-niwapo-chumbani-ni-mwendo-wa.html
true
939923276739022787
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago