Archive Pages Design$type=blogging

AUNT, ODAMA WATIMULIWA BONGO MOVIE

Hamida Hassan na Gladness Mallya UPEPO mbaya unaendelea kuvuma ndani ya Klabu ...

Hamida Hassan na Gladness Mallya
UPEPO mbaya unaendelea kuvuma ndani ya Klabu ya Bongo Movie Unity! Safari hii umewakumba mastaa wakubwa klabuni hapo, Devotha Mbaga, Aunt Ezekiel na Jennifer Kyaka ‘Odama’ ambao wanadaiwa kutimuliwa kundini kwa sababu ya kujiweka karibu na mwenyekiti wa klabu hiyo aliyejiuzulu, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’.
Mwanadada anaye tamba katika tasnia ya filamu bongo, Aunt Ezekiel
Kwa mujibu wa chanzo makini kilichozama katika kikao kilichofanyika juzikati, uongozi ambao ulibaki madarakani kundini baada ya Steve kujiuzulu, ulifanya tathmini upya ya memba waliobaki kisha kuwachuja hadi kubaki na wasanii 20 pekee wenye sifa.
“Wamewaengua baadhi ya wasanii ambao wameona hawana sifa ya kubaki kundini, miongoni mwao ni Devotha, Aunt na Odama. Wamesema wanahitaji mastaa wenye msimamo siyo kujipendekeza upande wa Steve, siku si nyingi watayaanika majina ya wenye sifa za kubaki kundini,” kilisema chanzo hicho.
Staa wa filamu bongo Devota Mbaga.
Chanzo hicho kilizidi kumwaga ‘ubuyu’ kuwa, wasanii walioenguliwa ni wanachama hai lakini si wanachama wenye msimamo na baadhi yao wameonesha udhaifu wa kuwa karibu na Steve Nyerere ambaye sasa anafanya harakati zake peke yake.
Baada ya habari hizo kutua katika rada ya Ijumaa, mapaparazi wetu waliwaendea hewani mastaa hao wakubwa waliodaiwa kufukuzwa, mambo yalikuwa hivi:
Mkali wa filamu Bongo, Jennifer Kyaka 'Odama'.
Devotha: Mimi ndiyo kwanza nakusikia wewe siku zote nipo nyumbani sijui hata habari za kikao hicho na sielewi wameniengua vipi wakati mimi ni mwanachama hai na ni miongoni mwa waanzilishi toka tulipokuwa watu saba, lakini kama wameamua hivyo sawa kwani siyo kwamba ukitoka ndiyo mwisho wa maisha.
Odama: Hakuna kitu kama hicho, wanaoenguliwa ni viongozi siyo wanachama, watanienguaje bila kunipa taarifa? Kwanza ndiyo nasikia sijui chochote ndiyo napata taarifa kutoka kwako.
Kwa upande wa Aunt Ezekiel, simu yake iliita bila kupokelewa.

COMMENTS

Name

Burudani Habari Hot News Magazeti Majuu Michezo Teknolojia/Movie Track (Audio & Video)
false
ltr
item
Tabasam Blog: AUNT, ODAMA WATIMULIWA BONGO MOVIE
AUNT, ODAMA WATIMULIWA BONGO MOVIE
http://api.ning.com:80/files/j-DiiE-nbb*Ah0QVYl6bQHAfO3SKnDBJsWI2ncX0v*kC0N6qpPa29q0HTT7PHnSr5vZcaKYbYf9Tiy3X7fRD0aUwBKVP72tb/AUNT.jpg?width=650
Tabasam Blog
https://tabasmtza.blogspot.com/2014/11/aunt-odama-watimuliwa-bongo-movie.html
https://tabasmtza.blogspot.com/
http://tabasmtza.blogspot.com/
http://tabasmtza.blogspot.com/2014/11/aunt-odama-watimuliwa-bongo-movie.html
true
939923276739022787
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago