Archive Pages Design$type=blogging

UBUNIFU HUONGEZA LADHA YA MAPENZI

Mu hali gani Mashosti zangu? Leo nimekuja kivingine tofauti na mlivyonizoea, sitaki kumchambua mtu, mtoto wa kike japo bila kumpasha md...

Mu hali gani Mashosti zangu? Leo nimekuja kivingine tofauti na mlivyonizoea, sitaki kumchambua mtu, mtoto wa kike japo bila kumpasha mdomo wangu huuona kama umechacha.
Waswahili wanasema raha ya ngoma kupokezana, siyo kung’ang’ania kuimba peke yako. Leo nimemkaribisha mgeni ambaye ni mtu wangu wa karibu hana tofauti na bata mzoefu wa kupata.
Leo mzungumzaji mkuu sijui nimwite shangingi wa kiume au kidume cha mbegu maana naye yumo katika kukimbizana na watoto wadogo, afadhali mwenzake nimepumua.
Nimekuwa nikijitahidi kuuzungumzia upande wa pili katika medani ya mahaba  kuhusu chakula cha nafsi lakini wapo wahusika wakuu ambao hawana tofauti na nyani mzee aliyepanda miti mingi. Sitaki kupoteza wakati ngoja nimkaribishe Babu Poa, Babu Poa karibu.
“Asante Bi Nasra au maarufu Bi Naa, siwezi kukuita shangingi mstaafu kwa vile bado unatoa huduma ndogondogo kwa wazee wenzio. Tuachane na hayo, leo nataka nizungumzie tabia za ubabe kwa wanaume kuwanyima uhuru wake zao kiasi cha kukidhi haja zao na kuwaacha wenzao njiani.
Katika lawama nyingi nilizozikuta kwa Bi Nasra ni kutokana na tabia za baadhi ya wanawake kuachwa njiani na waume zao. Kingine kutobadilishiwa mitindo ya kupeana mautamu.
Mwanamke akimwelekeza mumewe tufanye hivi unakuwa ugomvi, anamuona mwanamke si muaminifu, akishangaa eti amejuaje kubadili staili.Nataka niwaeleze wanaume wenzangu kitu kimoja katika kumfurahisha mpenzio ni kumfikisha safari yake na raha ya safari kufika si kuishia njiani.
Siku hizi unasikia mwanamke anashushiwa njiani na kufika mwenyewe kwa miguu (kukanda kwa maji ya moto). Mimi babu poa katika pilikapilika zangu za ujana nilikuwa siwezi kumuacha mwanamke njiani hata kama mimi nimewahi kufika nilikuwa siridhiki, lazima nitamsindikiza mwenzangu mpaka afike.
Uanaume si ndevu, kwani hata mbuzi anazo, bali kumkata kiu mpenzi wako, kama kula na kuvaa vyote hivyo alikuwa akivipata kwao. Lakini kuna kitu amekifuata kwako na si kingine ni bakora hata siku moja punda hafi kwa bakora.
Hakikisha kila ukimshika hakutaje jina lako na mwisho akupe asante, unamnyima raha unataka azipate wapi? Haya kila ukirudi na mtindo wako mmoja kama taa ya treni. Mpe raha mtoto wa watu, jamani kila kitu mpaka uambiwe hujui raha ya kilio ni machozi, utamlizaje bila kumtoa machozi.
Ukipanda juu ya mnazi usiteremke mpaka uhakikishe unamtupia madafu ya kutosha  mpaka akuambie ametosheka.
Hapa kidogo nataka nitoe somo kwa wanaume wenzangu, mapenzi si kumwaga mzigo na kuondoka, bali wote mfurahie mwenzako kwa kumfikisha na siku zote mwenye kutia chachu ya mapenzi ni mwanaume kwa utundu wake.
Hakuna shule ya mapenzi bali wewe mwenyewe kubuni vitu vya kumfurahisha mpenzi wako.
Wako wanaojifunza kupitia kanda za wakubwa, lakini kaka mkulima mzuri haangalii eneo lilivyo muhimu kuwepo na rutuba inayostawisha mbegu. Vivyo hivyo hata katika mapenzi mkao wowote wa mpenzi wako ni mtindo wa mapenzi.
Pia kama hujui mitindo usimfikirie vibaya mkeo kwani aliokuja nao huenda kaelekezwa na shoga zake ambao huenda ukapunguza mateso ya kuachwa njiani kila siku. Kwa hayo machache inatosha nakurudisheni kwa anti yenu.”
“Asante babu poa kumbe nawe una makombora mazito nina imani wamekusikia la muhimu kuyafanyia kazi.
Kwa leo inatosha tukutane wiki ijayo, ni mimi Anti yenu Nasra Shangingi Mstaafu.

COMMENTS

Name

Burudani Habari Hot News Magazeti Majuu Michezo Teknolojia/Movie Track (Audio & Video)
false
ltr
item
Tabasam Blog: UBUNIFU HUONGEZA LADHA YA MAPENZI
UBUNIFU HUONGEZA LADHA YA MAPENZI
http://api.ning.com:80/files/NDILiAzzLEUbmvdHjNGGAgpRSOztAVIde5o15825UFlW-J7ruE-nNhD4EKb*IQlkfSFQvSZ*obdR0e8auMR0XJYtisNSWkAE/shangi.jpg
Tabasam Blog
https://tabasmtza.blogspot.com/2014/10/ubunifu-huongeza-ladha-ya-mapenzi.html
https://tabasmtza.blogspot.com/
http://tabasmtza.blogspot.com/
http://tabasmtza.blogspot.com/2014/10/ubunifu-huongeza-ladha-ya-mapenzi.html
true
939923276739022787
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago