Archive Pages Design$type=blogging

Miss East Africa 2012 Joselyn Maro hajapewa kadi ya gari yake hadi leo, apeleka malalamiko BASATA

MSHINDI wa shindano la Miss East Africa kwa mwaka 2012, Joselyn Maro amepeleka malalamiko yake kwenye Baraza la...

MSHINDI wa shindano la Miss East Africa kwa mwaka 2012, Joselyn Maro amepeleka malalamiko yake kwenye Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) akilalamikia kutokabidhiwa nakala muhimu za zawadi yake ya gari alilopewa kama mshindi.
Ms eac Miss East Africa 2012 Joselyn Maro
Mrembo huyo alisema jana kuwa tangia apate ushindi wake huo alipewa gari aina ya Mazda ambalo hadi sasa hawezi kuliendesha kutokana na kutopewa kadi ya gari hilo. Alisema kuwa hali hiyo kwake imekuwa ni ya wasiwasi kwa kuwa amelazimika kuliegesha gari hilo nyumbani akisubilia kukamilika kwa nakala hizo.
Alisema kuwa amekuwa akilazimika kuwasiliana na mratibu wa shindano hilo kampuni ya Lena Events bila ya mafanikio yoyote. “Mimi nimekuwa nikimwomba kunisaidia suala hili la gari lakini ushirikiano umekuwa hakuna kabisa na niliamua kwenda Basata kuanzia mwezi Februari kuomba kusaidiwa na ndio ninasubiria majibu”alisema mrembo huyo.
Kwa upande wa Mkurugenzi wa Ukuzaji wa Sanaa wa Basata, Vivia Sharua alikiri kupokea malalamiko ya Miss huyo na kusisitiza kuwa ofisi yake imekuwa ikifanya jitihada za kumpata mwandaaji huyo bila ya mafanikio. “Sisi tumekuwa mara kwa mara tukimwandikia barua ya kumuita kwenye kikao lakini inaonekana kuwa amekuwa akituchenga”alisema Shalua.
“Hilo gari linathamani ya Dola za Kimarekani 18,000 ambazo mmiliki wa gari hilo naYe alikuja hapa Basata akilalamika kuwa hakupewa sehemu ya fedha za gari hilo kutoka kwa mwandaaji huyo na yeye anamdai huyo mwandaaji”.
Aliendelea kufafanua kuwa kutokana na kutolipwa kwa fedha zake mmiliki aliyetoa gari hili alilazimika kuzuia kadi ya gari ili lisiweze kuruhusiwa kutumika. Aliongeza kuwa baraza limeamua kumwandikia barua tena kwa mara ya mwisho mwandaaji huyo wa shindano hilo ikimwita katika kikao cha tathmini kitakachofanyika Septemba 24 mwaka huu katika ofisi za basata zilizopo Ilala.
Aliongeza kuwa kwa utaratibu mwandaaji wa shindano anatakiwa kukamilisha ripoti ndani ya mwezi mmoja tangia kumalizika kwa shindano lakini imekuwa tofauti kwa mwandaaji huyo ambapo kwa sasa ni takribani miaka miwili hajafika kwenye tathmini ya shindano lake.
“Kila akiitwa anakuwa na mambo yake mengine na hiyo imekuwa hivyo kuanzia mwaka 2012 sasa kwa sasa hivi Basata inae mwanasheria wake hivyo basi huo ndio mwisho wa huu ubabaishaji sisi tutalisimamia hadi huyo Miss apate haki yake,”alisema Vivia.
Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni inayoandaa shindano hilo, Lena Events Lena Calist alisema kuwa ofisi yake inaendelea kulishughulikia suala hilo. “Kamati yangu ya ufundi kwa sasa inaendelea na kulishughulikia suala hilo kwa na kila kitu kitakuwa sawa,”alisema Calist. Alisema kuwa aliwahi kuitwa Basata kipindi kilichopita na lakini hata hivyo alikuwa tayari kwenda kwenye kikao hicho kikaahirishwa.

COMMENTS

Name

Burudani Habari Hot News Magazeti Majuu Michezo Teknolojia/Movie Track (Audio & Video)
false
ltr
item
Tabasam Blog: Miss East Africa 2012 Joselyn Maro hajapewa kadi ya gari yake hadi leo, apeleka malalamiko BASATA
Miss East Africa 2012 Joselyn Maro hajapewa kadi ya gari yake hadi leo, apeleka malalamiko BASATA
http://www.bongo5.com/wp-content/uploads/2014/09/Ms-eac.jpg
Tabasam Blog
https://tabasmtza.blogspot.com/2014/09/miss-east-africa-2012-joselyn-maro.html
https://tabasmtza.blogspot.com/
http://tabasmtza.blogspot.com/
http://tabasmtza.blogspot.com/2014/09/miss-east-africa-2012-joselyn-maro.html
true
939923276739022787
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago