Archive Pages Design$type=blogging

Hivi Ndivyo Dudu Baya alivyofunguka na kusema "Sijaona nchi yenye wana Hip Hop fake kama Tanzania"

Msanii mkongwe wa Hip Hop nchini, Godfrey Tumaini aka Dudu Baya amedai kuwa amezunguka katika nchini kibao duni...

Msanii mkongwe wa Hip Hop nchini, Godfrey Tumaini aka Dudu Baya amedai kuwa amezunguka katika nchini kibao duniani lakini hajawahi kuona nchi yenye wasanii wa Hip Hop fake kama wa Tanzania.
Dudu Baya alikuwa kama surprise kwa mashabiki wa Tabora
Akizungumza jana, Dudu amesema aliwahi kujaribu kukutana na baadhi ya wasanii wa Hip Hop na kujadili baadhi ya changamoto zao ila ziligonga ukuta kutokana na uoga wao.
“Nimezunguka dunia nzima sijaona nchi yenye wana Hip Hop fake kama Tanzania,” amesema Dudu. “Yaani wana Hip Hop wa Tanzania ni fake, yaani hawajui maaana ya Hip Hop. Nilishawatafuta wengi tufanye harakati za kuokoa muziki wetu lakini nikiwafuata wanasema ‘aise bro hizi harakati ni ngumu’. Kama utakuwa unaona hata kutafuta haki yako ni ngumu utakufa ukiwa masikini kutokana na dosari za uzembe. Wewe unatakiwa uitetee jamii halafu unaogopa watu kwanini sasa uitwe mwana Hip Hop? Nilishawafuata wasinii wengi wa Hip Hop tutengeneze structure ya muziki wetu kibiashara lakini hawaeleweki. Nilishamfuata Professor, nilishakaa na Mwana FA, na nimeshakaa na wasanii wote wa Hip Hop unaowajua lakini wananiambia ‘bro hizi harakati zako hatuziwezi’,” amesema rapper huyo.
Katika hatua nyingine Dudu Baya amewataka wanawake wote ambao ni wadau kwenye burudani kuwasaidia wasanii wa kike wanaohitaji msaada.
“Unajua wanawake wanateseka sana kwenye hizi harakati za muziki wetu, tunahitaji kuwasaidia, kwa sababu presenter ili aicheze ngoma yake anahitaji kutoa rushwa ya ngono, producer pia, waandishi. Kwahiyo kiukweli wasanii wa kike wanahitaji kusaidiwa na wadau wa kike ambao wapo kwenye huu mtandao wa muziki. Kuna watangazaji kama akina DJ Fetty wapo wengi. Hao ndo wanatakiwa kuanzisha harakati za kuwasaidia wasanii wa kike. Nipo kwenye mchakato wa kuzungumza na baadhi ya wadau ili tujue tunajadili vipi ili kuwasaidia hawa ndugu zetu.”

COMMENTS

Name

Burudani Habari Hot News Magazeti Majuu Michezo Teknolojia/Movie Track (Audio & Video)
false
ltr
item
Tabasam Blog: Hivi Ndivyo Dudu Baya alivyofunguka na kusema "Sijaona nchi yenye wana Hip Hop fake kama Tanzania"
Hivi Ndivyo Dudu Baya alivyofunguka na kusema "Sijaona nchi yenye wana Hip Hop fake kama Tanzania"
http://www.bongo5.com/wp-content/uploads/2014/09/Dudu-Baya-alikuwa-kama-surprise-kwa-mashabiki-wa-Tabora.jpg
Tabasam Blog
https://tabasmtza.blogspot.com/2014/09/hivi-ndivyo-dudu-baya-alivyofunguka-na.html
https://tabasmtza.blogspot.com/
http://tabasmtza.blogspot.com/
http://tabasmtza.blogspot.com/2014/09/hivi-ndivyo-dudu-baya-alivyofunguka-na.html
true
939923276739022787
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago