Archive Pages Design$type=blogging

CHALZ BABA HATIMAYE AMEOMBA RADHI KWA MKEWE

  Mwanamuziki kiongozi wa bendi ya Mashujaa Musica, Charles Gabriel Baba, akiwa na mkewe. Stori: Shakoor Jongo MWANAMUZIKI ...

 Mwanamuziki kiongozi wa bendi ya Mashujaa Musica, Charles Gabriel Baba, akiwa na mkewe.

Stori: Shakoor Jongo
MWANAMUZIKI kiongozi wa bendi ya Mashujaa Musica, Charles Gabriel Baba, maarufu kama Chalz Baba, ambaye wiki iliyopita alimpa kipigo kikali mkewe, Rehema Sospeter na kusababisha ndoa yao kuyumba, hatimaye amemuomba radhi na hivi sasa wawili hao wamerejea kwenye uhusiano wao kama awali.

Habari zilizopatikana kutoka kwa chanzo makini, zinasema baada ya kutokea kwa varangati hilo, mke huyo aliahidi kurejea kwao kutokana na kuchoshwa na vipigo vya mara kwa mara kutoka kwa mwanamuziki huyo nyota wa zamani wa African Stars ‘Twanga Pepeta’.
Ilidaiwa kwamba baada ya tukio hilo, hata hali ya kiongozi huyo wa bendi haikuwa nzuri kisaikolojia, jambo lililofanya uongozi wa Mashujaa kuamua kuingilia kati ili kuiokoa ndoa hiyo.
Mmiliki wa Mashujaa Musica anayejulikana zaidi kwa jina la Mamaa Sakina, ndiye aliyefanya shughuli hiyo ya kusawazisha mambo kabla hayajaharibika zaidi.
Risasi Mchanganyiko lilifanikiwa kukutana na Mamaa Sakina katika ukumbi wa Ten Lounge uliopo Makumbusho jijini Dar es Salaam akiwa amekaa na mke wa mwimbaji huyo. Muda mchache baadaye Chalz Baba pia alitokea na moja kwa moja aliongoza kuelekea meza aliyokaa mkurugenzi huyo.
 
Chalz Baba,
“Ni kweli kabisa kama ulivyosikia, kwa sasa mimi na mke wangu tumemaliza tofauti zetu, nimemuomba radhi amenielewa, ile ahadi yake ya kutaka nimrudishe kwao ameifuta na sasa hivi tumeanza upya maisha yetu ya ndoa,” alisema Chalz Baba.
Naye kwa upande wake, Mamaa  Sakina alisema anamshukuru Mungu kuona ndoa hiyo imerejea kwani isingekuwa vizuri kuona imevunjika.“Sasa hivi Chalz na mkewe kama unavyowaona, mahaba tele wamemaliza tofauti zao,” alisema.
SAJENTI NUSURA ATIBUE HALI YA HEWA
Wakati mambo yakionekana kunyooka, ghafla hali nusura ibadilike baada ya zilipendwa wa Chalz ambaye alibahatika kuzaa naye mtoto mmoja wa kike anayejulikana kwa jina la Husna Idd ‘Sajenti’ kwenda mbele kumtunza mwanamuziki huyo alipokuwa akifanya makamuzi jukwaani.
Kitendo hicho kilidaiwa kumuudhi Rehema ambaye alijikuta akinuna ghafla hasa baada ya Chalz kutabasamu kwa kutunzwa na Sajenti.

COMMENTS

Name

Burudani Habari Hot News Magazeti Majuu Michezo Teknolojia/Movie Track (Audio & Video)
false
ltr
item
Tabasam Blog: CHALZ BABA HATIMAYE AMEOMBA RADHI KWA MKEWE
CHALZ BABA HATIMAYE AMEOMBA RADHI KWA MKEWE
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgMqAnd15_1nFXXk1yLj6V5yB0yux3eTAgCaoY7l3IwLr9c1p7xVlHeGuUwuCJzpSA2qqzhu9aWahF7o1DUsc48yol5dDPkl8i2GW2ZpZo_Svse5gvwhiopeDsaYQIrJ_99urwoTF9_sO4/s1600/chaznamkewe.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgMqAnd15_1nFXXk1yLj6V5yB0yux3eTAgCaoY7l3IwLr9c1p7xVlHeGuUwuCJzpSA2qqzhu9aWahF7o1DUsc48yol5dDPkl8i2GW2ZpZo_Svse5gvwhiopeDsaYQIrJ_99urwoTF9_sO4/s72-c/chaznamkewe.JPG
Tabasam Blog
https://tabasmtza.blogspot.com/2014/09/chalz-baba-hatimaye-ameomba-radhi-kwa.html
https://tabasmtza.blogspot.com/
http://tabasmtza.blogspot.com/
http://tabasmtza.blogspot.com/2014/09/chalz-baba-hatimaye-ameomba-radhi-kwa.html
true
939923276739022787
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago