Archive Pages Design$type=blogging

ANAYEDAIWA MCHAWI ADONDOKEA KANISANI

NIkweli imetokea! Ni kwenye Kanisa la Paradise Internation Ministries lililoko Karakata Ukonga jijini Dar, mwanamke mmoja (pichani) ana...

NIkweli imetokea! Ni kwenye Kanisa la Paradise Internation Ministries lililoko Karakata Ukonga jijini Dar, mwanamke mmoja (pichani) anayedaiwa mchawi alidondoka usiku wa saa saba na kujikuta hawezi kutembea.
Mwanamke anayedaiwa kuwa mchawi akiwa amedondoka Kanisani.
Tukio hilo lilijiri Septemba 13, mwaka huu wakati waumini wa kanisa hilo wakiwa wamezama kwenye maombi ya kufunga.
Ilidaiwa kuwa, waumini wa kanisa hilo wakiwa katika maombi hayo, Nabii Gideon Parapanda aliwahakikishia kuwa usiku huo kutatokea mambo ya ajabu kufuatia maombi hayo.
Inadaiwa ilipofika saa saba usiku mwanamke huyo akiwa na wenzake watatu, walidondokea kanisani hapo na kusababisha taharuki kwa waumini waliokuwa wakifanya maombi ndani. Mwanamke huyo alikuwa na kitambaa chekundu kikidaiwa ni hirizi, fimbo  nyeusi iliyozungushiwa shanga na alikuwa amejipaka masizi mwilini.
Mwanamke baada ya kudondokea kanisani na kusababisha taharuki kwa waumini waliokuwa wakifanya maombi ndani. 
Akizungumza na Uwazi, Nabii Parapanda alisema watu hao walidondoka watatu, wawili walifanikiwa kukimbia akabaki huyo mmoja aliyejitambulishwa kwa jina moja la Aisha, mkazi wa Mwananyamala A jijini Dar.
Baada ya tukio hilo vyombo vya ulinzi, askari wa JWTZ na polisi walifika kwa lengo la kuhakikisha usalama wa eneo  hilo lakini nabii huyo aliomba mtu huyo asichukuliwe hadi atapofanyiwa maombi maalum.
Ombi la kiongozi huyo lilikubaliwa ambapo Aisha alipandishwa  madhabahuni na kukiri kuwa alikuwa na wenzake watano lakini katika kuanguka walikuwa watatu, wawili walifanikiwa kukimbia bila kusema walikuwa wakitoka wapi kwenda wapi.
Kitambaa chekundu alichokuwa nacho mwanamke huyo.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Ilala, SACP Mary Nzuki alipohojiwa kuhusiana na tukio hilo alisema:
“Ni kweli tukio hilo limetokea na watu wameshuhudia, mwanamke huyo bado  yuko kanisani hapo kwa maombi.”

COMMENTS

Name

Burudani Habari Hot News Magazeti Majuu Michezo Teknolojia/Movie Track (Audio & Video)
false
ltr
item
Tabasam Blog: ANAYEDAIWA MCHAWI ADONDOKEA KANISANI
ANAYEDAIWA MCHAWI ADONDOKEA KANISANI
http://api.ning.com:80/files/YkTQKvQouurm6ekwcOA6ihPLzqneGPWK28wIaiZjde2YbEuMCuATMnHr*IftjRrIPonnOBNOzLBgaxoaA5SzwCJf6T0KOfJ6/7.jpg?width=650
Tabasam Blog
https://tabasmtza.blogspot.com/2014/09/anayedaiwa-mchawi-adondokea-kanisani.html
https://tabasmtza.blogspot.com/
http://tabasmtza.blogspot.com/
http://tabasmtza.blogspot.com/2014/09/anayedaiwa-mchawi-adondokea-kanisani.html
true
939923276739022787
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago