Archive Pages Design$type=blogging

2mbili wa Town: Kundi jipya la Baba Levo na Peter Msechu litakalotambulishwa hivi karibuni

Muungano wa wasanii wawili wacheshi na wenye vituko kutoka Kigoma, Peter Msechu na Baba Levo hivi sasa utakuwa ...

Muungano wa wasanii wawili wacheshi na wenye vituko kutoka Kigoma, Peter Msechu na Baba Levo hivi sasa utakuwa ukitambulika kwa jina moja la ‘2mbili Wa Town’.
peter na baba levo
Wasanii hao ambao ukibahatika kukutana nao ni ngumu kuondoka bila kuvunja mbavu zako, wanatarajia kutambulisha project yao mpya ya pamoja ya ‘2mbili wa Town’ hivi karibuni.
“Jina la project linaitwa Tumbili wa town, so kuna vitu vingi ndani ya hiyo project, sema bado hatujaamua kuielezea project nzima mambo yake ya ndani na vitu vilivyo kwasababu kuna mshindo mkubwa unakuja wakati wa kutambulisha hiyo project.”
Baba Levo ameongea leo
Baba Levo amesema ‘Tumbili Wa Town’ ni kundi la watu wawili yeye na Peter Msechu litakalokuwa likifanya mambo mengi.
“Kwanza kwa kifupi ni kama kundi, ni kundi la watu wawili sema sasa kuna vitu ambavyo tutakuja kuvifanya ambavyo ni vitu vikubwa sana sana kwenye hii industry ya muziki, movie na vitu kama hivyo. So ni kwasababu hatujakuwa rasmi kwaajili ya kuielezea hiyo project ndio maana unaona tunakuwa tunaielezea juu juu , kutokana na watu wanaoisimamia project kusema wanataka wahakikishe vitu vyote vimekaa sawa sawa and then sasa ndio tuitambulishe watu wote wajue ni kitu gani,” alisema Baba Levo.
Ameongeza kuwa licha ya kuungana na Peter Msechu kwaajili ya project hiyo lakini kila mmoja bado ataendelea na project zake binafsi za muziki walizokuwa wakizifanya toka zamani.
“Hii project haiwezi kutufanya tusiendelee na project zetu ambazo tumekuwa nazo kuanzia mwanzo, bado tutaendelea kuwa na brand zetu zile zile kama Baba Levo, kama Peter Msechu lakini kwa pamoja tunatengeneza Tumbili Wa Town”.
Naye Peter Msechu kupitia Instagram aliandika kuhusu project hiyo:
“and our official name is “2MBILI WA TOWN” more project to come ya all stay tuned…. we on point this year no jokes at all… wengine mnatutukana ni sawa tunashukuru wengine mnafurahi tunachokifanya pia tunawashukuru.. tunachoamini ni kila mmoja anajua namna anavyo tafuta ugali wake.. hii ni yetu ili mradi hatuibi wala kukaba mtu basi tunamshukuru Mungu..”
Baba Levo alimaliza kwa kusema kuwa ndani ya wiki mbili au tatu zijazo project ya Tumbili Wa Town itatambulishwa.

COMMENTS

Name

Burudani Habari Hot News Magazeti Majuu Michezo Teknolojia/Movie Track (Audio & Video)
false
ltr
item
Tabasam Blog: 2mbili wa Town: Kundi jipya la Baba Levo na Peter Msechu litakalotambulishwa hivi karibuni
2mbili wa Town: Kundi jipya la Baba Levo na Peter Msechu litakalotambulishwa hivi karibuni
http://www.bongo5.com/wp-content/uploads/2014/09/peter-na-baba-levo.jpg
Tabasam Blog
https://tabasmtza.blogspot.com/2014/09/2mbili-wa-town-kundi-jipya-la-baba-levo.html
https://tabasmtza.blogspot.com/
http://tabasmtza.blogspot.com/
http://tabasmtza.blogspot.com/2014/09/2mbili-wa-town-kundi-jipya-la-baba-levo.html
true
939923276739022787
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago