Archive Pages Design$type=blogging

OWINO NAHODHA MPYA SIMBA SC, KISIGA MSAIDIZI WAKE, CHOLLO AVULIWA BEJI BAADA YA KUPOTEZA NAMBA ‘FIRST ELEVEN’

BEKI Mganda, Joseph Owino ameteuliwa kuwa Nahodha wa Simba SC, nafasi iliyokuwa inashikiliwa na Nassor Masoud ‘Chollo’ ambay...

BEKI Mganda, Joseph Owino ameteuliwa kuwa Nahodha wa Simba SC, nafasi iliyokuwa inashikiliwa na Nassor Masoud ‘Chollo’ ambaye amepoteza namba mbele ya kocha mpya, Mzambia Patrick Phiri.  
Phiri alimuanzisha katika mchezo mmoja tu wa kirafiki Chollo dhidi ya Kilimani, ambao ndio ulikuwa wa kwanza kwa timu hiyo katika kambi yake ya Zanzibar, lakini tangu hapo amekuwa akimpanga kinda Miraj Adam. 
Baada ya Miraj kufanya vizuri katika mechi dhidi ya Mafunzo na KMKM, Phiri ameamua kuteua viongozi wapya wa wachezaji wenzao, Owino akiwa Nahodha Mkuu na Shaaban Kisiga ‘Malone’ akiteuliwa kuwa Nahodha Msaidizi. 
Bosi wa wachezaji; Joseph Owino ameteuliwa kuwa Nahodha mpya Simba SC
Owino akiwatambulisha wachezaji wa Simba SC kwa mgeni rasmi jana Uwanja wa Amaan

Simba SC imeweka kambi visiwani Zanzibar kujiandaa na msimu mpya wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, unaotarajiwa kuanza Septemba 20, mwaka huu.
Pamoja na kufanya mazoezi, Simba SC imecheza mechi tatu za kujipima nguvu hadi sasa, dhidi ya Kilimani waliyoshinda 2-1, Mafunzo 2-0 na KMKM 5-0, zote Uwanja wa Amaan.
Ligi Kuu inatarajiwa kuanza Septemba 20, mwaka huu, mabingwa watetezi wakianza na Polisi Morogoro Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam Septemba 20, mwaka huu, wakati Yanga SC waliomaliza nafasi ya pili wataanza na Mtibwa Sugar Uwanja wa Jamhuri, Morogoro siku hiyo.
Washindi wa tatu, Mbeya City wataanza na JKT Ruvu ya Pwani, Uwanja wa Sokoine, Mbeya Septemba 20 na washindi wa nne, Simba SC wataanza na Coastal Union ya Tanga Septemba 21, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Mechi nyingine za ufunguzi za Ligi Kuu zitakuwa kati ya Stand United watakaoikaribisha Ndanda ya Mtwara Uwanja wa Kambarage, Shinyanga, Mgambo JKT wataikaribisha Kagera Sugar Uwanja wa Mkwakwani, Tanga na Ruvu Shooting watakuwa wenyeji wa Prisons Uwanja wa Mabatini, Mlandizi mkoani Pwani.
Naodha Msaidizi; Shaaban Kisiga 'Melone' amerudi na mguu mzuri Simba SC

COMMENTS

Name

Burudani Habari Hot News Magazeti Majuu Michezo Teknolojia/Movie Track (Audio & Video)
false
ltr
item
Tabasam Blog: OWINO NAHODHA MPYA SIMBA SC, KISIGA MSAIDIZI WAKE, CHOLLO AVULIWA BEJI BAADA YA KUPOTEZA NAMBA ‘FIRST ELEVEN’
OWINO NAHODHA MPYA SIMBA SC, KISIGA MSAIDIZI WAKE, CHOLLO AVULIWA BEJI BAADA YA KUPOTEZA NAMBA ‘FIRST ELEVEN’
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg0vGvNeIki5pj4CsIVXg086lmakiffr28vspAWUhMSMPcMqetUkTPPnlAmeJOU7EMJpNrLEmSK1y_8yRi6HdXnAKkxLsTUnwcuXOOxKU94YxSFK3Oc-LJ10o8wnRrw4C8lC1UvFciXUFen/s1600/OWIINO.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg0vGvNeIki5pj4CsIVXg086lmakiffr28vspAWUhMSMPcMqetUkTPPnlAmeJOU7EMJpNrLEmSK1y_8yRi6HdXnAKkxLsTUnwcuXOOxKU94YxSFK3Oc-LJ10o8wnRrw4C8lC1UvFciXUFen/s72-c/OWIINO.jpg
Tabasam Blog
https://tabasmtza.blogspot.com/2014/08/owino-nahodha-mpya-simba-sc-kisiga.html
https://tabasmtza.blogspot.com/
http://tabasmtza.blogspot.com/
http://tabasmtza.blogspot.com/2014/08/owino-nahodha-mpya-simba-sc-kisiga.html
true
939923276739022787
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago