Mwimbaji wa Bongo Flava aliyewahi kuwa mshiriki wa shindano la Kuimba BSS, Meninah La Diva amefanya exclusive Interview ...
Mwimbaji wa Bongo Flava aliyewahi kuwa mshiriki wa shindano la Kuimba
BSS, Meninah La Diva amefanya exclusive Interview na tovuti ya Times Fm
na kufunguka mengi ambayo hakuwahi kuyasema.
Katika mahojiano hayo aliyofanya na Josefly Muhozi, amezungumzia
kuhusu kipindi chake kipya cha runinga kitakachoanza hivi karibuni.
Amezungumzia pia kilichojiri baada ya kusambaa ripoti kuwa anatoka na
Diamond Platinumz na anavyomchukulia Wema Sepetu.
Kuhusu Muziki wake, Meninah ambaye hivi sasa ameachia ‘Pipi ya
Kijiti’ ameeleza ugumu na mipango alinayo katika kuvuka mipaka na
kufanikiwa zaidi.
Kuhusu Mapenzi, mwimbaji huyo amemzungumzia mumewe mtarajiwa na mwimbaji wa kiume ambaye kwa ‘ndoto’ zake anaota angekuwa mpenzi wake ‘kokote uliko kama unanisikia, I Love You’...! Sikiliza hapo chini akimtaja na kumpa ujumbe.
Meninah ambaye anasomea uandishi wa habari na utangazaji, ameeleza
anachokifahamu kuhusu uwepo wa rushwa ya ngono kwenye media kati ya
baadhi ya watu wa media na wasanii wa kike na ushauri wake.
Isikilize hapa, hupaswi kuikosa hii Interview.. Credit za kutosha kwa DJ RGuy wa 100.5 Times Fm.