Archive Pages Design$type=blogging

Huyu Ndio Nyota aliyejisomesha kwa kuuza vitumbua, vyuma chakavu(4)

  Wiki iliyopita Nature alielezea ujio wa kundi jipya la Wanaume Halisi baada ya kuvunjika kwa Kundi la Wanaume Family. ...

 
Wiki iliyopita Nature alielezea ujio wa kundi jipya la Wanaume Halisi baada ya kuvunjika kwa Kundi la Wanaume Family.
Wiki hii pamoja na mambo mengine, nguli huyo wa muziki wa kizazi kipya anaeleza jinsi alivyopata wakati mgumu kutunga mashairi na hali ya muziki ilivyo.
Anaeleza kuwa iliwachukua siku nyingi kutunga mashairi la wimbo mmoja na kwamba walifanya hivyo ili zidumu, hivyo shairi moja lilikuwa likimchukua hadi mwezi mzima kukamilisha kulitunga.
“Labda uwezo wetu ulikuwa mdogo, naona siku hizi mtu anatunga nyimbo 12 kwa siku. Mimi huwa nashangaa sana, au msanii mchanga anakwambia ana albamu nne ingawa inasikika kwa singo moja,”anasema Nature.
Anasema kuwa ugumu wa kazi hiyo ulimfanya hata augue homa kila alipomaliza kutunga nyimbo za albamu, kutokana na uchovu uliotokana na kuishughulisha akili bila kutaka kubugudhiwa. Nature anaeleza kuwa ilifikia wakati alikwenda kushinda ufukweni mwa bahari ili kukimbia marafiki ambao wangemsumbua wakati anatunga mashairi.
“Hakuna albamu niliyotunga bila kupata homa, hasa ya ‘Ugali’ ndiyo niliumwa sana, ndiyo sababu nikiona mtu ametunga nyimbo zaidi ya 10 kwa siku, namshangaa na kuona ana uwezo sana, “anasema Nature.
Nature anazungumzia utunzi wa sasa na mapokeo ya mashabiki akisema kuwa watunzi wengi hurudia ujumbe kutokana na kukosa umakini na kuiga, hivyo kutodumu na kuyeyuka mapema mioyoni mwa mashabiki.
Anafafanua kuwa wasanii wengi wa muziki kwa sasa wanaamini wakiimba singo moja watakuwa matajiri kutokana na kuwaona baadhi ya wanamuziki wamefanikiwa na wao kutamani hali hiyo, lakini matokeo yake wanaboronga.
Anaitaja changamoto wanakumbana nayo wasanii kwa sasa kuwa ni wanaojiita wadau wa muziki wa kizazi kipya kuwatumia vibaya wasanii na wanang’amua wanatumiwa, hupotezwa katika sanaa.
Anasema hali hiyo imekuwa inawaondoa kwenye soko wasanii mahiri kwa sababu watu wanaowaamini huwanyonya na kuwaacha hoi.
“Hapa nawataka wasanii wenzangu kuwa makini na watu hawa wanaojifanya wanapenda kuendeleza muziki na wasanii kwani mwishowe huwapoteza makusudi katika sanaa ili kujilinda wasionekane wabaya, “anasema.
Kuhusu kuwapo kwa studio nyingi za muziki ikiwamo ya kwake ( Halisi Recods), Nature alisema kuwa zinaleta ushindani unaozaa kazi bora
- Mwananchi

COMMENTS

Name

Burudani Habari Hot News Magazeti Majuu Michezo Teknolojia/Movie Track (Audio & Video)
false
ltr
item
Tabasam Blog: Huyu Ndio Nyota aliyejisomesha kwa kuuza vitumbua, vyuma chakavu(4)
Huyu Ndio Nyota aliyejisomesha kwa kuuza vitumbua, vyuma chakavu(4)
http://www.mwananchi.co.tz/image/view/-/2421076/highRes/810250/-/maxw/600/-/unu36dz/-/nature.jpg
Tabasam Blog
https://tabasmtza.blogspot.com/2014/08/huyu-ndio-nyota-aliyejisomesha-kwa.html
https://tabasmtza.blogspot.com/
http://tabasmtza.blogspot.com/
http://tabasmtza.blogspot.com/2014/08/huyu-ndio-nyota-aliyejisomesha-kwa.html
true
939923276739022787
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago