Archive Pages Design$type=blogging

SHULE KUTIMUA WATUMIA VIPODOZI NA WAVAA MLEGEZO

Shule ya Sekondari Mwadui iliyopo wilayani Kishapu mkoani Shinyanga, imetangaza kufukuza wanafunzi wote wanaotumia vipodozi, wanaovaa ...

Shule ya Sekondari Mwadui iliyopo wilayani Kishapu mkoani Shinyanga, imetangaza kufukuza wanafunzi wote wanaotumia vipodozi, wanaovaa sketi fupi, milegezo na wanaotumia simu za mkononi shuleni.
Mwalimu Mkuu wa shule hiyo inayomilikiwa na Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria, Mchungaji Yohana Nzelu, alisema hayo jana katika kikao cha Bodi ya Shule na Wazazi.
Mwalimu Nzelu alisema moja ya chachu ya mafanikio ya wanafunzi shuleni, ni nidhamu ya kutosha na maadili mema na kuongeza kuwa Bodi hiyo ilikaa na kujadili namna ya kuongeza ufaulu kwa wanafunzi wake na kuweka mikakati, ikiwemo hatua hizo.
Akisoma taarifa kwa wazazi na walezi wa wanafunzi walio katika shule hiyo, Mwalimu Nzelu alisema hatua hizo zinalenga kuzuia wanafunzi kujiingiza katika makundi mabaya na kuboresha taaluma.
‘’Shule hii katika matokeo ya Mtihani wa Taifa wa Kidato cha Nne mwaka 2012, wanafunzi 61 waliopata daraja la kwanza mpaka la tatu na mwanafunzi mmoja alichaguliwa kwenda kidato cha tano.”
‘’Mwaka jana (2013) wanafunzi 76 walifanya mtihani wa kidato cha nne, waliopata daraja la kwanza mpaka la tatu 33, waliochaguliwa na Serikali kujiunga kidato cha tano wanafunzi 24, na waliokwenda shule binafsi walikuwa saba.
 “Tumepiga hatua hivyo mikakati iliyopo ni kusisitiza maadili na kuondoa changamoto zilizokuwepo za wanafunzi kukosa nidhamu,“ alieleza Mwalimu Nzelu.
Akizungumza kwenye kikao hicho, Askofu Mkuu wa KKKT  Dayosisi hiyo, Emmanuel Makala, ambaye ndiye msimamizi wa shule hiyo, alisema suala hilo si la kupuuzwa na hawatakuwa na msamaha kwa mwanafuzi atakayekiuka sheria hizo huku akitoa mwito kwa wazazi na walezi kushirikiana kwa pamoja.
Askofu Makala alisema wazazi na walezi wakishirikiana ipasavyo na walimu kwa kufuatilia taarifa za watoto wao shuleni, itasaidia kwa kiwango kikubwa kuongeza taaluma ya wanafunzi na kupata ufaulu mzuri.

COMMENTS

Name

Burudani Habari Hot News Magazeti Majuu Michezo Teknolojia/Movie Track (Audio & Video)
false
ltr
item
Tabasam Blog: SHULE KUTIMUA WATUMIA VIPODOZI NA WAVAA MLEGEZO
SHULE KUTIMUA WATUMIA VIPODOZI NA WAVAA MLEGEZO
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh2GcA5NeRsoiLDtxjakHvl2QZam_m9aFt8Oim7BPeuUhpGgHrlOaD8gzDBWymHkN3CexGFPyiEu7jz6c9wQ8YE5rTmWwZeHMn_cxcWBGKgrtv5fH6wOze7dOrhve6QAEzH3-9Iht9TeDo/s1600/shule.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh2GcA5NeRsoiLDtxjakHvl2QZam_m9aFt8Oim7BPeuUhpGgHrlOaD8gzDBWymHkN3CexGFPyiEu7jz6c9wQ8YE5rTmWwZeHMn_cxcWBGKgrtv5fH6wOze7dOrhve6QAEzH3-9Iht9TeDo/s72-c/shule.jpg
Tabasam Blog
https://tabasmtza.blogspot.com/2014/07/shule-kutimua-watumia-vipodozi-na-wavaa.html
https://tabasmtza.blogspot.com/
http://tabasmtza.blogspot.com/
http://tabasmtza.blogspot.com/2014/07/shule-kutimua-watumia-vipodozi-na-wavaa.html
true
939923276739022787
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago