Archive Pages Design$type=blogging

SIO MUDA MUAFAKA WA KUMUITA COUTINHO MUUZA MADAFU KUTOKA BRAZIL

...


Afisa habari wa Yanga sc, Baraka Kizuguto (kushoto) akiwa na Coutinho (kulia) baada ya kuwasili  nchini  jana akitokea kwao nchini Brazil.
YANGA SC imemsajili kiungo mshambuliaji kutoka nchini Brazil, Andrey Marcel Ferreira Coutinho.
 
Mchezaji huyo aliwasili jana mchana jijini Dar es salaam akitokea kwao nchini Brazil tayari kwa kuanza kazi ya kuitumikia Yanga katika msimu wa 2014/2014 wa ligi kuu soka Tanzania bara.
 
Coutinho aliwaeleza waandishi wa habari kuwa anajisikia furaha kuwa Tanzania, nchi ambayo watu wake wanapenda mpira.
 
Mchezaji huyo haijui Tanzania, lakini ameifahamu kutokana na bosi wake Marcio Maximo ambaye amechangia kwa asilimia zote kumleta nchini.
 
Bila shaka wakati wanaongea na Maximo juu ya kuja kufanya kazi Tanzania, Coutinho alihoji mambo mengi na mazingira ya Tanzania na kupewa majibu na Maximo ambaye unaweza kusema ni mwenyeji wake.
 
Maximo anafahamu utamaduni wa mashabiki wa Tanzania na alimweleza ukweli kiungo huyo na yeye kuiamini Tanzania mpaka kusema anafurahia kufanya kazi kwenye ardhi ya nchi hii ya Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete.
 
Brazil kuna wachezaji wengi na vipaji vingi vya soka. Hii ni nchi inayosemekana kunukia mpira kila kona.
 
Tunaona wabrazil wengi wanafanya makubwa katika soka la sasa duniani, lakini miaka ya nyuma walitokea wachezaji wakali pia.
Unamkumbuka Pele? Huko mbali, miaka ya karibuni tu, akina Ronaldo, Ronaldinho, Ricardo Kaka`, Robinho, na sasa Neymar wametikisa soka la dunia.
 
Hawa ni mfano tu, ukiamua kuwataja wachezaji wa Brazil waliofanya kazi nzuri utaandika kwa muda mrefu na huwezi kumaliza,  lakini ninachojaribu kusema ni kwamba, Brazil ni nchi yenye vipaji vingi vya soka.
 
Kwa wale waliobahatika kufika Brazil, wanajua wazi kuhusu hilo. Ukipita mitaa mingi ya nchi hii, lazima uwakute vijana wanacheza soka.
 
Katika maelezo ya Coutinho alisema amewahi kucheza barani Asia na alipata uzoefu mzuri, hivyo anaamini chini ya makocha aliowazoea ataisaidia Yanga.
 
Kucheza Asia sio jambo jepesi, huko pia kuna mpira na watu wana mipango mizuri. chanzo BARAKA MPENJA

COMMENTS

Name

Burudani Habari Hot News Magazeti Majuu Michezo Teknolojia/Movie Track (Audio & Video)
false
ltr
item
Tabasam Blog: SIO MUDA MUAFAKA WA KUMUITA COUTINHO MUUZA MADAFU KUTOKA BRAZIL
SIO MUDA MUAFAKA WA KUMUITA COUTINHO MUUZA MADAFU KUTOKA BRAZIL
https://fbcdn-sphotos-f-a.akamaihd.net/hphotos-ak-xpf1/t1.0-9/10352837_10204420994232057_1327726715607196512_n.jpg
Tabasam Blog
https://tabasmtza.blogspot.com/2014/06/sio-muda-muafaka-wa-kumuita-coutinho.html
https://tabasmtza.blogspot.com/
http://tabasmtza.blogspot.com/
http://tabasmtza.blogspot.com/2014/06/sio-muda-muafaka-wa-kumuita-coutinho.html
true
939923276739022787
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago