Archive Pages Design$type=blogging

SEKRETARIETI YA AJIRA YABAINI VYETI 1,035 VYA KUGHUSHI

Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma imeshabaini   vyeti vya kughushi   1,035 kutoka kwa baadhi ya waombaji   kazi tangu   mpa...

Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma imeshabaini  vyeti vya kughushi  1,035 kutoka kwa baadhi ya waombaji  kazi tangu  mpango wa kuhakiki vyeti ulipoanza hadi  mwezi  Mei mwaka huu.
Hayo yamesemwa na Msemaji wa Sekretarieti ya Ajira, Riziki Abraham  kwenye Maonesho ya Utumishi wa Umma, yanayoendelea katika Viwanja vya Mnazi Mmoja, jijini Dar es Salaam. Riziki alisema katika vyeti hivyo vya kughushi vilivyobainika, 661 ni vyeti vya shule za sekondari, ambavyo wahusika wanadai kuvipata kutoka Baraza la Taifa la Mitihani (NECTA), leseni  tatu za udereva, vyeti 257  vya udereva, ambavyo wahusika wanadai kuvipata kutoka vyuo vya Mafunzo ya Ufundi (VETA) na Chuo cha Taifa cha Usafirishaji(NIT), vyeti 86 vya kuzaliwa na vyeti 28 vya taasisi mbalimbali.
Pia, alisema katika mwaka wa fedha wa 2013/14, Sekretarieti ya Ajira, ilifanikiwa kujaza  nafasi sita za maofisa watendaji wakuu, nafasi 65 za wakurugenzi na wakuu wa idara na nafasi 27 za wakuu wa vitengo wa Wakala wa Serikali na taasisi za umma.
Riziki alisema Sekretarieti  ya Ajira katika Utumishi wa Umma, inatumia njia mbalimbali katika kuwasiliana na wadau wake, ikiwemo kutoa taarifa za uendeshaji wa mchakato wa ajira serikalini. 
“Matangazo  ya kazi na taarifa mbalimbali hutolewa kupitia vyombo mbalimbali vya habari, kama vile tovuti ya Sekretarieti ya Ajira ambayo ni   www.ajira.go.tz, ukurasa wa face book  wa ‘Sekretarieti  ajira’, runinga, redio, magazeti, majarida, vipeperushi  na ushiriki katika semina  na kongamano  mbalimbali,” alisema.

COMMENTS

Name

Burudani Habari Hot News Magazeti Majuu Michezo Teknolojia/Movie Track (Audio & Video)
false
ltr
item
Tabasam Blog: SEKRETARIETI YA AJIRA YABAINI VYETI 1,035 VYA KUGHUSHI
SEKRETARIETI YA AJIRA YABAINI VYETI 1,035 VYA KUGHUSHI
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiHhKiisVAmvtxJZG6HWFcYbGKeY9M2X6u003hNQDKF6FvJLmlhzvocZ4yQtwNGsKX3zHfKl5KbooskiLdeiCpPF2OI0_mS-9dyQ6jDXmidQr5yuyJjv5Nd4aDnGCrJ3-KBMtNoiJSWxNs/s1600/ajira.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiHhKiisVAmvtxJZG6HWFcYbGKeY9M2X6u003hNQDKF6FvJLmlhzvocZ4yQtwNGsKX3zHfKl5KbooskiLdeiCpPF2OI0_mS-9dyQ6jDXmidQr5yuyJjv5Nd4aDnGCrJ3-KBMtNoiJSWxNs/s72-c/ajira.jpg
Tabasam Blog
https://tabasmtza.blogspot.com/2014/06/sekretarieti-ya-ajira-yabaini-vyeti.html
https://tabasmtza.blogspot.com/
http://tabasmtza.blogspot.com/
http://tabasmtza.blogspot.com/2014/06/sekretarieti-ya-ajira-yabaini-vyeti.html
true
939923276739022787
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago