KAMA kawa kama dawa, ndani ya Exclusive Interview leo tupo naye muigizaji mkongwe w...
KAMA
kawa kama dawa, ndani ya Exclusive Interview leo tupo naye muigizaji
mkongwe wa sinema za Kibongo, Sabrina Rupia ‘Cathy’ ambaye alianza sanaa
tangu enzi za makundi hadi zilipofika zama za kurekodi sinema.
Mwandishi: Umeanza kitambo sanaa, umri wako unaonekana ni mkubwa, je una miaka mingapi, kabila na umezaliwa wapi?
Cathy: Tafadhali sipendi kuanika mwaka wangu, ila mimi ni Mpare na nimezaliwa Kijiji cha Lembeni mkoani Kilimanjaro.
Mwandishi: Vipi kuhusu elimu yako? Cathy: Elimu yangu ni ya kawaida sana, si kubwa ya kusema nikaajiriwe kwenye kampuni, kwanza siwezi kuajiriwa hata kwa mtu kwa sababu nina mambo mengi sana ya kufanya. Mwandishi: Kwa nini hutaki kuajiriwa?
Cathy: Mimi ni mtu wa kukimbizana na hela siwezi kukaa kwa mtu au kwenye ofisi nikisubiri mwisho wa mwezi.
Mwandishi: Wewe ni mtoto wa ngapi kwenu? Cathy: Mtoto wa nane katika familia ya mzee Rupia mwenye watoto 11, mimi na mwenzangu tulizaliwa mapacha.
Mwandishi: Cathy ni mtu wa aina gani? Cathy: Watu wanavyosema niko ni mcheshi, nina huruma sana, namwamini Mungu katika kila jambo, napenda amani, mtu wa watu napenda kujumuika na wenzangu bila kujali kipato, elimu kabila wala rangi, sidharau mtu yeyote na ndiyo maana niko kwenye vikundi vya kina mama wajasiriamali na vikundi hivi vina kila tabaka la watu.
Mwandishi: Jirani zako wanadai unajiona ni kweli? Cathy: Si kweli kila mtu Mtoni Kijichi (anapoishi) ni rafiki yangu, nawapenda na wao wananipenda sema huwezi kupendwa na kila mtu na mara nyingi watu wa hivyo huwa hawana sababu maalum ya kumchukia mtu ukimuuliza atakwambia , simpendi tu.
Mwandishi: Unapenda kitu gani katika maisha yako? Cathy: Napenda amani na kuambiwa ukweli pale ninapokosea kwani naamini nitakuwa nimejifunza kitu kipya na sitorudia kosa la kwanza.
Mwandishi: Wapare wana sifa gani? Cathy: (Hapa anajivutia kwake) wapole sana na mara nyingi wamama wa Kipare ni wachapakazi ndiyo maana hata mimi nilipoanza kujitegemea sikuwa na shida kwani niliamini mafunzo ya kazi nilizopitia wakati niko nyumbani zilinifanya nijiamini kuwa naweza kuishi kwa kutegemea kazi ya mikono yangu.
Mwandishi: Ulianza kujitegemea ukiwa na umri gani?
Cathy: Kiukweli nilianza kujitegema nikiwa mdogo sana kama miaka kumi na kitu hivi, hata kumi na nane sikufikisha, nilikuwa bado sijakomaa kabisa.
Mwandishi: Daah! Ulikuwa mdogo sana, ulitoroka nyumbani au ulitoroshwa?
Usikose wiki ijayo kujua ili kujua sababu zilizomfanya Cathy ajitegemee akiwa na umri mdogo.
- gpl
Muigizaji mkongwe wa sinema za Kibongo, Sabrina Rupia ‘Cathy’
Alifanikiwa kuanza kutengeneza jina lake katika Kundi la Mambo Hayo
na baadaye Kaole. Hapa chini amezungumza vitu vingi na mwandishi wetu,
tujiunge naye:Mwandishi: Umeanza kitambo sanaa, umri wako unaonekana ni mkubwa, je una miaka mingapi, kabila na umezaliwa wapi?
Cathy: Tafadhali sipendi kuanika mwaka wangu, ila mimi ni Mpare na nimezaliwa Kijiji cha Lembeni mkoani Kilimanjaro.
Mwandishi: Vipi kuhusu elimu yako? Cathy: Elimu yangu ni ya kawaida sana, si kubwa ya kusema nikaajiriwe kwenye kampuni, kwanza siwezi kuajiriwa hata kwa mtu kwa sababu nina mambo mengi sana ya kufanya. Mwandishi: Kwa nini hutaki kuajiriwa?
Cathy: Mimi ni mtu wa kukimbizana na hela siwezi kukaa kwa mtu au kwenye ofisi nikisubiri mwisho wa mwezi.
Mwandishi: Wewe ni mtoto wa ngapi kwenu? Cathy: Mtoto wa nane katika familia ya mzee Rupia mwenye watoto 11, mimi na mwenzangu tulizaliwa mapacha.
Mwandishi: Cathy ni mtu wa aina gani? Cathy: Watu wanavyosema niko ni mcheshi, nina huruma sana, namwamini Mungu katika kila jambo, napenda amani, mtu wa watu napenda kujumuika na wenzangu bila kujali kipato, elimu kabila wala rangi, sidharau mtu yeyote na ndiyo maana niko kwenye vikundi vya kina mama wajasiriamali na vikundi hivi vina kila tabaka la watu.
Mwandishi: Jirani zako wanadai unajiona ni kweli? Cathy: Si kweli kila mtu Mtoni Kijichi (anapoishi) ni rafiki yangu, nawapenda na wao wananipenda sema huwezi kupendwa na kila mtu na mara nyingi watu wa hivyo huwa hawana sababu maalum ya kumchukia mtu ukimuuliza atakwambia , simpendi tu.
Mwandishi: Unapenda kitu gani katika maisha yako? Cathy: Napenda amani na kuambiwa ukweli pale ninapokosea kwani naamini nitakuwa nimejifunza kitu kipya na sitorudia kosa la kwanza.
Mwandishi: Wapare wana sifa gani? Cathy: (Hapa anajivutia kwake) wapole sana na mara nyingi wamama wa Kipare ni wachapakazi ndiyo maana hata mimi nilipoanza kujitegemea sikuwa na shida kwani niliamini mafunzo ya kazi nilizopitia wakati niko nyumbani zilinifanya nijiamini kuwa naweza kuishi kwa kutegemea kazi ya mikono yangu.
Mwandishi: Ulianza kujitegemea ukiwa na umri gani?
Cathy: Kiukweli nilianza kujitegema nikiwa mdogo sana kama miaka kumi na kitu hivi, hata kumi na nane sikufikisha, nilikuwa bado sijakomaa kabisa.
Mwandishi: Daah! Ulikuwa mdogo sana, ulitoroka nyumbani au ulitoroshwa?
Usikose wiki ijayo kujua ili kujua sababu zilizomfanya Cathy ajitegemee akiwa na umri mdogo.
- gpl