post-feature-image
HomeHabari

Wahadzabe walia na hujuma za wanaume

Arusha. Katika jamii nyingi, hasa za mijini, ni kawaida wanawake na wanaume kushirikiana katika shughuli mbalimbali za kiuch...

Breaking News:- Mama Mzazi wa Zitto Kabwe Afariki
New Track:- #4 Sugua Gaga Refix - Shaa Feat Lamar
NASRY - NiNi (OFFICIAL MUSIC VIDEO) PRODUCED BY: BOB MANECKY VIDE

Arusha. Katika jamii nyingi, hasa za mijini, ni kawaida wanawake na wanaume kushirikiana katika shughuli mbalimbali za kiuchumi.
Lakini hali hii ni tofauti kwa Wanawake wa jamii za pembezoni za wafugaji; Wamasai, Wabaebeig na Wahadzabe ambao wanaume wao badala ya kuwaunga mkono katika miradi yao, wamekuwa wakiwahujumu. 
Baadhi ya wanaume hawa wamefikia hatua ya kupora mifugo, ya vikundi vya akina mama hawa, ili wasiendelee kiuchumi.
Wanawake wa jamii hizo, wakizungumza na Mwananchi katika mkutano uliokuwa umeandaliwa na mtandao wa mashirika ya wafugaji na waokota matunda (PINGOS Forums), wanasema miradi yao imekufa baada ya kuhujumiwa na waume zao.
Amina Msendekwa, mfugaji kutoka jamii ya Wamasai wa Kijiji cha Wami Sokoine wilayani Mvomelo, anasema mradi wao wa kunenepesha mifugo katika kijiji chao umekwama baada ya wanaume wao kuiba mifugo kabla ya mauzo ili wasiendelee na biashara hiyo.
Anasema walianzisha mradi huo baada ya kupata hamasa na elimu ya kutosha, hivyo wakawa wananunua ndama wadogo na kuwafuga kwa kuwanenepesha na baadaye kujipanga kuuza ng'ombe wakubwa.
"Mradi wetu ulikuwa mzuri sana. Tulinenepesha mifugo, lakini tulipopanga kuuza baada ya kukamilika, tulianza kuibiwa kidogo kidogo," anasema.
Kutokana na majukumu yao kama wanawake, iliwalazimu kuomba msaada kwa wanaume kuwasaidia kuwasaka ng'ombe waliokuwa wanaibiwa, lakini cha ajabu walikuwa hawapewi ushirikiano na baadaye walibaini ni njama za waume zao.
"kila tulipokuwa tukipanga kupeleka ng'ombe mnadani, waliibiwa na wanaume zetu na jitihada za kurejeshewa zilikwama hadi sasa mradi umekufa," anasema Msendekwa.
Paulina Tipapu, mkazi wa Loliondo, anasema licha ya mtandao wa mashirika yasiyo ya kiserikali wilaya ya Ngorongoro wa Nngonet kuwapa mbuzi watano wa kisasa, mradi huo umekwamishwa na wanaume.
Tipapu anasema wanaume wamekuwa wakichukuwa mbuzi bila idhini yao na kwenda kuwauza na hata pale wanapokwenda wao kuuza wanaume wamekuwa waking'ang'ania fedha.
"Tumeshindwa kuendeleza mradi kama tulivyotarajia baada ya waume zetu kutuhujumu. Sasa tunakaa kubuni miradi mingine," anasema Tipapu. 
Chanzo Mwananchi
Name

Burudani Habari Hot News Magazeti Majuu Michezo Teknolojia/Movie Track (Audio & Video)
false
ltr
item
Tabasam Blog: Wahadzabe walia na hujuma za wanaume
Wahadzabe walia na hujuma za wanaume
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjwiLF45kRjSy3qoXgx2ELo6SufkEeyKZ9duKp6HRLBHO0uUOYN3YPDSRkgVoEuMtiQk_3haaTGZ5zUp0PdMWe-T-6ZoAVUfp5_am7krAZqionlKHY75Fb-19GDs2NvAis8H68TQZJCU-th/s640/03++Hadzabe+fire+making.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjwiLF45kRjSy3qoXgx2ELo6SufkEeyKZ9duKp6HRLBHO0uUOYN3YPDSRkgVoEuMtiQk_3haaTGZ5zUp0PdMWe-T-6ZoAVUfp5_am7krAZqionlKHY75Fb-19GDs2NvAis8H68TQZJCU-th/s72-c/03++Hadzabe+fire+making.jpg
Tabasam Blog
https://tabasmtza.blogspot.com/2014/05/wahadzabe-walia-na-hujuma-za-wanaume.html
https://tabasmtza.blogspot.com/
http://tabasmtza.blogspot.com/
http://tabasmtza.blogspot.com/2014/05/wahadzabe-walia-na-hujuma-za-wanaume.html
true
939923276739022787
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago