Archive Pages Design$type=blogging

Simba yakataa usajili wa Logarusic

KAMATI ya Utendaji ya Simba, imeikataa ripoti ya kocha wao, Mcroatia, Zdravko Logarusic inayoonyesha ni wachezaji wangapi anataka kuw...

KAMATI ya Utendaji ya Simba, imeikataa ripoti ya kocha wao, Mcroatia, Zdravko Logarusic inayoonyesha ni wachezaji wangapi anataka kuwasajili na wangapi anataka kuwatema.
Logarusic amerejea kwao kwa ajili ya mapumziko baada ya Ligi Kuu Bara kumalizika.
Hiyo ni siku chache tangu kamati hiyo kukutana kupitia ripoti ya usajili ya timu hiyo aliyoikabidhi hivi karibuni kabla ya kurejea kwao Croatia akisubiria mkataba mpya wa kuendelea kukinoa kikosi hicho kilichomaliza ligi kikiwa nafasi ya nne.
Kwa mujibu wa taarifa zilizofika kwenye meza ya Championi Jumatatu, ripoti ya kocha huyo imewakataa wachezaji 17 kati ya 30 waliosajiliwa msimu uliopita na inaonyesha kwamba kati ya hao, wanatakiwa wabaki 13 tu.
Hii ina maana kuwa Simba sasa watatakiwa kusajiliwa wachezaji wengine 17 kama inavyoonyesha kwenye ripoti ya Logarusic, jambo ambalo kamati imelikataa.
Kamati hiyo imekataa kuwaondoa wachezaji wote hao kutokana na wengi wao kubakiza mikataba ya mwaka mmoja, hivyo ili wasitishe mikataba yao basi lazima wawalipe fedha.
“Tumeipitia vizuri ripoti ya kocha aliyoikabidhi kwenye kamati ya utendaji na kuona baadhi ya upungufu uliopo, hali inayotupa ugumu wa usajili kwa ajili ya msimu ujao.
“Ukiangalia ripoti hiyo inataka wachezaji 17 wasitishiwe mikataba yao kwa kile anachodai kuwa hawana uwezo wa kubaki kuendelea kuichezea Simba.
“Kati ya hao 17 basi ni watatu au wanne ambao wenyewe mikataba yao ndiyo imemalizika na hao wengine mikataba yao wamebakiza ya mwaka mmoja, hivyo kama kamati tunaona ni vyema tukawabakiza baadhi ya wachezaji kwa hofu ya kuingia hasara ya kulipa fedha nyingi kwa ajili ya kuvunja mikataba.
“Kwanza kuwasajili wachezaji 17 ili idadi kamili itimie litakuwa jambo gumu sana kwetu,” alisema mtoa taarifa huyo aliyekataa katakata kutajwa jina lake na Championi Jumatatu likaheshimu hilo.
Alipoulizwa Katibu Mkuu wa Simba, Ezekiel Kamwaga, alisema: “Bado kamati ya utendaji na ya usajili zinaendelea kupitia ripoti ya mapendekezo ya kocha aliyoiacha, hivyo tusubirie mara baada ya kukamilika kila kitu kitawekwa wazi.”

COMMENTS

Name

Burudani Habari Hot News Magazeti Majuu Michezo Teknolojia/Movie Track (Audio & Video)
false
ltr
item
Tabasam Blog: Simba yakataa usajili wa Logarusic
Simba yakataa usajili wa Logarusic
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEicB9x7qyc6a2WkJYwQIJbbjoyMiCc6LIVvnV3cXbxPLyYQmvhRPaJ5iMxU8wOyKo18lhDoHs_91R4RLEsNlt7fVAlNZhHkdLf4Xafx9MUBM0ywdLIW-Rq0NWASdevCgNc1IxtY6vVHbgk/s1600/nembo-ya-simba.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEicB9x7qyc6a2WkJYwQIJbbjoyMiCc6LIVvnV3cXbxPLyYQmvhRPaJ5iMxU8wOyKo18lhDoHs_91R4RLEsNlt7fVAlNZhHkdLf4Xafx9MUBM0ywdLIW-Rq0NWASdevCgNc1IxtY6vVHbgk/s72-c/nembo-ya-simba.jpg
Tabasam Blog
https://tabasmtza.blogspot.com/2014/05/simba-yakataa-usajili-wa-logarusic.html
https://tabasmtza.blogspot.com/
http://tabasmtza.blogspot.com/
http://tabasmtza.blogspot.com/2014/05/simba-yakataa-usajili-wa-logarusic.html
true
939923276739022787
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago