Archive Pages Design$type=blogging

HIVI NDIVYO PICHA ZA UTUPU ZILIVYOMTESA NORA

Tunaendelea kupata mtiririko wa mahojiano ya mwingizaji Nuru Nasoro ‘Nora’ tuliyoanza wiki iliyopita, karibu: Mwigizaji mkongwe wa tasni...

Tunaendelea kupata mtiririko wa mahojiano ya mwingizaji Nuru Nasoro ‘Nora’ tuliyoanza wiki iliyopita, karibu:
Mwigizaji mkongwe wa tasnia ya filamu za kibongo Nuru Nasoro ‘Nora’
Gladness: Unawaambia nini wenzako wenye tabia hizo chafu za kutembea na watu ovyo?
Nora: Mimi nawaasa waachane na tabia hiyo kwani magonjwa ni mengi ukizingatia kuwa wanaume wenyewe wanawatumia tu kama vyombo vya starehe.

Gladness: Ni kitu gani ambacho kimewahi kukuumiza sana katika maisha yako?
Nora: Ukweli picha za utupu ziliniumiza sana kwani zilikuwa ni mbinu za wasanii wenzangu kutaka kunishusha kisanaa ambapo walinipiga nikiwa nimelala sijielewi.
Gladness: Huwa unaenda msikitini?

Nora: Ndiyo, mara mojamoja kwani mara nyingi huwa naswali nyumbani kwa siku mara tano.
Gladness: Kwa nini msikitini mara mojamoja?

Nora: Dini yetu inaruhusu mwanamke kuswali nyumbani kwani ndiyo anapata thawabu zaidi.
Gladness: Uliwahi kuwa na bifu na Vincent Kigos ‘Ray’ na Blandina Chagula ‘Johari’, je kwa sasa mkoje?
Nora: Mimi nilishawatangazia msamaha kwa yote mabaya waliyonitendea, Johari huwa tunaongea lakini Ray sijawahi kuongea naye.

Gladness: Zamani uliwahi kuwa kichaa na kupotea kabisa kwenye fani, je unayazungumziaje maisha hayo ya nyuma?
Nora: Huwa sitaka kuyakumbuka kwa sababu yananisikitisha sana, nilipoteza muda mwingi sana na kurudishwa nyuma kimaendeleo.
Gladness: Ni mafanikio gani uliyoyapata kwenye sanaa mpaka sasa?
Nora: Sijapata mafanikio yoyote zaidi ya kujulikana kwa sababu sanaa ya Tanzania bado iko nyuma, hailipi kihivyo kama watu wanavyofikiria.

Gladness: Nini sababu za kuachana na mume wako wa kwanza, marehemu Ng’wizukulu Jilala?
Nora: Huwa sipendi kuzungumzia sana hilo ila kilichosababisha mimi kuachana na mume wangu wa kwanza ni kwamba alikuwa akinitesa sana yaani nilikuwa nashushiwa kipigo kila kukicha.
Gladness: Je, ulipewa talaka au uliamua kuondoka tu mwenyewe?

Nora: Ukweli baada ya kuona mateso yamenizidi niliomba talaka mwenyewe lakini aliitoa kwa nguvu baada ya wazazi wangu kuingilia kati.
Gladness: Ulifanikiwa kuzaa naye watoto wangapi?

Nora: Nilifanikiwa kuzaa naye mtoto mmoja tu ambaye ndiye niliye naye mpaka sasa.
Gladness: Tuachane na mume wa kwanza tuje kwa huyu wa pili (Luqman), nataka kujua je, yeye hukufanikiwa kuzaa naye?

Nora: Hatukufanikiwa kuzaa, nami sikuwa tayari kuzaa naye kwa sababu kuna vitu ambavyo vilikuwa havijatimia.
Gladness: Baada ya kuachana na Luqman uliingia kwenye uhusiano wa kimapenzi na msanii mwenzako Geofrey na mliahidi kwamba mtaoana lakini mkaachana, nini sababu?
Nora: Mimi sikuwahi kuwa na uhusiano na Geofrey yule alikuwa ni meneja wangu na tulikuwa tukishirikiana katika kazi.

Gladness: Je kwa sasa una mchumba au mpenzi?
Nora: Sina mpenzi wala mchumba.

Gladness: Wewe ni mwanamke uliyekamilika unawezaje kuzuia tamaa za mwili wakati hauna mpenzi?
Nora: Huwa ninafanya mazoezi sana hivyo naweza kuzizuia tamaa hizo za mwili.
Gladness: Je una mpango wa kuzaa tena?

Nora: Ndio, nikishaolewa nitazaa lakini siwezi kuzaa nje ya ndoa.
Gladness: Je unahitaji mwanaume wa aina gani?
Nora: Namuhitaji mwanaume atakayenipenda mimi Nuru na siyo Nora, mwenye mapenzi ya kweli, atakayeniweka mimi mbele kwenye kila jambo, anayejishughulisha kimaisha, mtanashati na anayemuogopa Mungu.

Gladness: Turudi nyuma kidogo kwenye kipindi ambacho uliugua sana na kuwa kichaa, je ni wasanii gani waliokuwa bega kwa bega na wewe?
Nora: Hakuna hata mmoja aliyekuja hata kuniona zaidi walikuwa wakinikandamiza.

Mwisho!
-GPL

COMMENTS

Name

Burudani Habari Hot News Magazeti Majuu Michezo Teknolojia/Movie Track (Audio & Video)
false
ltr
item
Tabasam Blog: HIVI NDIVYO PICHA ZA UTUPU ZILIVYOMTESA NORA
HIVI NDIVYO PICHA ZA UTUPU ZILIVYOMTESA NORA
http://api.ning.com:80/files/Q7T2q86GkzWdC7FDH0jtnry1-KrpN2WpEne8bbegK17lAfHS-2fszWCUOLPHyvaoV6sCxWApjWXE47FeG0wDdTfSOOYXdt53/norabc.jpg?width=650
Tabasam Blog
https://tabasmtza.blogspot.com/2014/05/hivi-ndivyo-picha-za-utupu-zilivyomtesa.html
https://tabasmtza.blogspot.com/
http://tabasmtza.blogspot.com/
http://tabasmtza.blogspot.com/2014/05/hivi-ndivyo-picha-za-utupu-zilivyomtesa.html
true
939923276739022787
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago