post-feature-image
HomeBurudani

SHOGA, SI KILA BIASHARA MATANGAZO!

JAMANI mwishowe nitapasuka mdomo kwa kusema, mambo mengine kwa mwanamke aibu kuyafanya. Mnakuwa kama hamkwenda mkoleni mkafundwa mkafund...

JAMANI mwishowe nitapasuka mdomo kwa kusema, mambo mengine kwa mwanamke aibu kuyafanya. Mnakuwa kama hamkwenda mkoleni mkafundwa mkafundika. Hata kama hukwenda bado una aibu ya kike, mnakimbilia mambo ya kuiga ndiyo maana ndoa za siku hizi zimekosa neema wala maisha marefu.
Nani alikwambia kicheni pati ya siku moja unafunda mtu  kama siyo kukupoteza na kukupeleka siko. Si wajinga walianzisha mafunzo ya mwanamke ya kuujua uanamke wake na thamani yake. Pia kujua mwanaume umfanyie vitu gani apagawe na kuwaona wanawake wa nje si mali kitu.
Kujua viungo nyeti vya mwanamke viko wapi,  anatakiwa avae nguo ipi ili izibe sehemu gani, lakini leo hii kila mtu anajiendea bora liende, mnatia aibu mbayaaa eeeeh.
Kweli sisi wanawake wa sasa hamnazo ili hali tunazo, tumekuwa kila jambo tunaiga, jamani siyo kila kitu kipya lazima mwanamke akifanye au akipate, wakati kila siku unaenda peke yako, huendi na mtu.
Leo nataka niwapashe tena wapashike, wanawake wasio na haya kufanya mambo ya chumbani barabarani eti kwenda na wakati, wapiii? Nimeshakueleza wakati hauendi na mtu, wewe tu na kujifanya unajua kumbe unaungua na jua.
Jamani sasa hivi tembea barabarani utakutana na wanawake, vya siri vimewekwa hadharani, maumbile yote ambayo hatakiwi kuyaona mtu zaidi ya mwandani wako,  imekuwa sasa hivi hayafichwi tena. Najiuliza hivi jamani wanawake sasa hivi uanamke wetu hatuujui?
Kama inafika hatua unatembea na vazi linalomfanya mwanamke mwenzako aone aibu, ujue umevuka ubinaadamu, sasa hivi ni mnyama kasoro mkia. Sifa ya mnyama ni kufanya mambo bila kufikiri wala kuona aibu, ndiyo maana mnyama anaweza kutembea na mama yake bila wasi na kumzalisha na atakayezaliwa atatembea na bibi yake bila wasi!
Lakini kwa sisi wanadamu ukifanya hivyo litakuwa gumzo la mwaka na kila mmoja atakulaani.
Sasa hivi mjini hajulikani nani changu nani mke wa mtu wala nani yupo kwa wazazi wake.
Ni vululuvululu, mavazi wanayovaa machangu usiku kutafutia wateja ndiyo mavazi ya wasichana na kina mama mchana, mbona aibu. Jamani tatizo nini kufikia hatua ya kugeuka mahayawani na akili tunazo!
Nani aliyekuambia sifa ya mwanamke kwa mwanaume ni kutembea kwa kuyaacha maumbile nyeti kila mtu ayaone, bila kujali anayeona ni mtoto mdogo au mzee. Sasa hivi kuziona shanga, nguo za ndani ni jambo la kawaida hata matiti nje!
Mmh! Kweli kazi ipo wazazi wana kazi ya ziada kwa watoto wa kike. Ndani ya daladala unamkuta mtu kavaa suruali isiyo na mkanda ndani kavaa bikini na anaimana bila wasiwasi. Unajiuliza mtu huyo na mbuzi wana tofauti gani!
Huenda mnaamini kufanya hivyo ndiyo njia ya kumnasa mwanaume, basi mnajidanganya. Muoaji hawezi kukuchukua kwa kuamini wewe si mwanamke sahihi baada ya kuuona mwili wako hatakuwa na kitu anachokitaka zaidi ya kuyatamani maumbile yako kisha kufanya mapenzi na wewe na kukuacha.
Kwa mtindo huu wa kutembea uchi mkidhani ndiyo njia ya kumpata mwanaume mtakuwa mnajidanganya zaidi ya kugeuzwa Big G utatafunwa na kutemwa.
Hata kama ukiwa mtaalamu wa mapenzi, huwezi kuolewa zaidi ya watu kubadilishana na kukuacha akionekana huna maana na kuwa jamvi la wageni. Ndiyo maana kuna wasichana wazuri wenye sifa lakini mpaka leo hawaolewi kutokana na kuwa na sifa mbaya.
Jamani si kila biashara inataka matangazo, mengine ni kujidhalilisha.
Hebu badilikeni, yafunikeni maumbile yenu ili wanaume wavutike kuwaoa, mwanaume pamoja na kupenda  umbile zuri lakini kikubwa wanaangalia sana tabia. Kwa leo yanatosha tukutane wiki ijayo.
Ni mimi anti Nasra Shangingi Mstaafu.
- GPL 
Name

Burudani Habari Hot News Magazeti Majuu Michezo Teknolojia/Movie Track (Audio & Video)
false
ltr
item
Tabasam Blog: SHOGA, SI KILA BIASHARA MATANGAZO!
SHOGA, SI KILA BIASHARA MATANGAZO!
http://api.ning.com:80/files/pM3ABSV3WVULz7-vuYie7sit1Yn2gZSGF92onSg7u*X6QJbsm7Qf5HggjWZXFdPkp-wNy9L*6NvMiwuQQkBnQ8ypZ6wgjLXd/uditagoswami.jpg?width=650
Tabasam Blog
https://tabasmtza.blogspot.com/2014/04/shoga-si-kila-biashara-matangazo.html
https://tabasmtza.blogspot.com/
http://tabasmtza.blogspot.com/
http://tabasmtza.blogspot.com/2014/04/shoga-si-kila-biashara-matangazo.html
true
939923276739022787
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago